Blogger Widgets

December 12, 2013

Unaijua Hii Bahati ya Ali Kiba ikiwemo na Kesho kuwa mgeni Rasmi Uswisi

Star wa muziki wa Bongofleva kutoka Tanzania Ali Kiba kesho Ijumaa tarehe 13/12/2013 atakuwa na show huko Uswisi na mgeni maalum wa show hiyo atakuwa ni Ashley Toto ambaye ni promota wa wasanii wa Africa mashariki hususani nchini Ujerumani anakoishi. Ashley pia ni muigizaji wa filamu za kiswahili katika nchi za Scandinavia akiwa na asili ya Kenya. Ali Kiba alifanya show Ujerumani wiki iliyopita ambayo iliandaliwa na Ashley na wenzake nchini Ujerumani na kesho Ali Kiba atakuwa na show nyingine nchini Uswisi baada ya kuunganishwa na Ashley na promota wa huko. Akizungumza na Swahilihood Ashley alisema "Show ya German alifanya last Saturday na yuko na nyingine ambayo am the special quest in Swiss,  ya Swiss mimi ndio nimemuunganishia na promoter wa huko na hii ya Germany nilikua na wenzangu tuliandaa"


                                                   Ali Kiba na Ashley Toto

No comments:

Post a Comment