Kama ulishangaa kusikia kuwa Diamond Platnumz alilipa dola 5,000
ili kumshirikisha Davido kwenye remix ya My Number One, huenda
ukaishiwa nguvu kusikia kiwango kinachodaiwa kutolewa na msanii wa
Nigeria, KCEE ili kufanya collabo na first lady wa YMCMB, Nicki Minaj.
Kuna tetesi kuwa KCEE amelipa kitita cha N68m, ambazo ni zaidi ya
shilingi milioni 675 za Tanzania ili amshirikishe malkia huyo mpya wa
hip hop nchini Marekani. Kufuatia tetesi hiyo, meneja wa KCEE, Soso
Sobrekon, ameongea na mtandao wa NET kufafanua mambo yalivyo.
“Tupo nchini Marekani kujaribu kupata collaboration. Ni kweli tupo
kwenye mchakato wa kufanya wimbo na Nicki Minaj. Tulitaka kuifanya iwe
surprise kwa mashabiki lakini kwakuwa tayari imejulikana, tunataka
kuifanya iwe kuwa zaidi,” alisema.
Hata hivyo meneja huyo alikataa kuthibitisha kama kweli kiwango hicho
ndicho walicholipa. “Tunataka kumuongeza msanii mwingine wa YMCMB
ambaye ni mkubwa kuliko Nicki Minaj. Nicki ameshathibitishwa kuwa kwenye
wimbo huo, lakini kwakuwa sasa kila mtu anafahamu, bado tutawasurprise
mashabiki kwa kumchukua msanii mwingine kutoka YMCMB.’
No comments:
Post a Comment