Honolina akijitahidi kufukuza nzi waliojazana kwenye vidonda vyake
Kutokana na ugonjwa huo wa ajabu macho ya mtoto huyo yamekufa
Nyama la pili mfano wa pembe lililoota mgongoni
Bi,Grece John mama mzazi wa mtoto huyo ambaye amekubali kukatwa makalio yake ili mwanaye apone
Honalina akinywa maji baada ya kupigwa na jua kali alipokuwa akiomba sendi ya mabasi msamvu Morogoro wiki iliyopita
Mpiga debe huyo baada ya kumuona live mtoto huyo alishindwa kujizuia na kumwaga machopzi hadharani
Wananchi wakimchangia mama huyo
Honolina mbaye ugonjwa huo umeababisha miguu yake kuishiwa nguvu na kushindwa kusimama
Mwandishi
wa habari hizi ambaye anaifuatilia kwa karibu famili hiyo mwaka Mach 17
2012 alifika wodi namba 4 hospital ya mkoa wa Morogoro na kumkuta mama
huyo akiwa amelazwa na mtoto wake huyo ambaye wakti huo manya makubwa
yalikuwa bado hayajaanza kumtoka kama anavyooneka pichani,aliyepakatwa
na mtoto wa mwisho wa mama huyo.
Na Dustan Shekidele,Morogoro.
LAZIMA
utokwe machozi! Grace John mkazi wa Mzumbe, Mvomero mkoani Morogoro yupo
kwenye wakati mgumu kutokana na maradhi ya ajabu yanayomsumbua mwanaye
Honolina Christian Mkude (11).
Honolina
anasumbuliwa na ugonjwa wa kuota nyama sehemu za mwili wake zinazofanana
na pembe za mnyama, ugonjwa ambao unamtesa tangu kuzaliwa kwake.
ILIKUWAJE?
Akisimulia kisa kizima, mama mzazi wa Honolina, Bi. Grace, anasema tangu amemzaa mwanaye huyo ni mitihani baada ya mitihani.
Akisimulia kisa kizima, mama mzazi wa Honolina, Bi. Grace, anasema tangu amemzaa mwanaye huyo ni mitihani baada ya mitihani.
Mazungumzo
hayo yalifanyika hivi karibuni katika kituo cha mabasi ya mikoani,
Msamvu, mjini hapa wakati mama huyo na mwanaye wakihangaikia kuchangisha
fedha za usafiri wa kwenda Moshi kutafuta tiba zaidi katika Hospitali
ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC).
“Ndugu
mwandishi, kwa kweli sijui hatima ya mwanangu. Nilimzaa akiwa ameota
nywele sehemu zote za mwili wake, hadi usoni. Mimi na mume wangu
tulishangaa, lakini tuliendelea na matibabu katika hospitali mbalimbali
maana baadaye alianza kupatwa na uvimbe.
MTIHANI MWINGINE
“Jamani ndugu yangu... Mungu ana mitihani yake. Mume wangu (Christian Mkude) ambaye ndiye alikuwa tegemeo pekee kwetu, alifariki mwaka 2007 kwa ajali ya gari, wakati akisaka fedha za matibabu ya mwanetu.
“Jamani ndugu yangu... Mungu ana mitihani yake. Mume wangu (Christian Mkude) ambaye ndiye alikuwa tegemeo pekee kwetu, alifariki mwaka 2007 kwa ajali ya gari, wakati akisaka fedha za matibabu ya mwanetu.
“Kifo
chake, kwangu kimekuwa pigo mujalabu. Sina pa kukimbilia na hivi juzi tu
tulikuwa tumelazwa Hospitali ya Mkoa (Morogoro) na hapo tumepewa barua
ya kwenda KCMC kwa matibabu zaidi.
“Hivi
unavyoniona nachangisha fedha ili nipate angalau nauli za kutufikisha
kwanza hospitalini. Nimechanganyikiwa kabisa,” alisema Bi. Grace kwa
majonzi na kuongeza:
“Wakati
tatizo la mwanangu linaanza sikutegemea kama siku moja angekuja kuwa
hivi. Zilianza kuota nywele mwili mzima, baadaye vidonda vikaanza
kumtoka na sasa hali imebadilika na kuota nyama hizi kubwa kama mapembe
kama unavyoona.”
SAUTI YA BI. GRACE KUTOKA MOSHI
Juzi mwandishi wa habari hizi ambaye anaendelea kuifuatilia familia hiyo alimpigia simu Bi,Grece kwalengo la kujua kama wamefika salama,"Mungu akubariki sana kwa kutupigania tunamshukuru mungu tumefika salama,Misaada ya fedha kidogo tuliopata pele stenzi za daladala na ile ya Msamvu kutoka kwa wasamaria wema Msamvu, ilitusaidi kusafiri hadi Moshi na kufika katika Hospitali ya KCMC''alisema mama huyo.
Juzi mwandishi wa habari hizi ambaye anaendelea kuifuatilia familia hiyo alimpigia simu Bi,Grece kwalengo la kujua kama wamefika salama,"Mungu akubariki sana kwa kutupigania tunamshukuru mungu tumefika salama,Misaada ya fedha kidogo tuliopata pele stenzi za daladala na ile ya Msamvu kutoka kwa wasamaria wema Msamvu, ilitusaidi kusafiri hadi Moshi na kufika katika Hospitali ya KCMC''alisema mama huyo.
BADO ANAHITAJI MSAADA
“Madaktari wametupa moyo, wamesema watajaribu kumsaidia mwanangu. Watamtoa hizo nyama ila kwa sababu kutabaki na mashimo lazima wapandikize nyama nyingine.
“Tumeshakubaliana kuwa mimi ndiye nitakayekatwa sehemu ya nyama kutoka kwenye makalio yangu kwa ajili ya kumsaidia mwanangu,” alisema Bi. Grace, kilio kikisikika kwenye simu.
“Madaktari wametupa moyo, wamesema watajaribu kumsaidia mwanangu. Watamtoa hizo nyama ila kwa sababu kutabaki na mashimo lazima wapandikize nyama nyingine.
“Tumeshakubaliana kuwa mimi ndiye nitakayekatwa sehemu ya nyama kutoka kwenye makalio yangu kwa ajili ya kumsaidia mwanangu,” alisema Bi. Grace, kilio kikisikika kwenye simu.
Akaongeza:
“Wameshachukua nyama za mwanangu na kwenda kupima na baadaye watachukua
zangu ili kuona kama zinaendana, upasuaji ufanyike. Gharama kwa ajili
ya matibabu hayo wamesema ni shilingi 400,000 na mimi sina uwezo.
“Watanzania wenzangu, naombeni mnisaidie ili niweze kuondokana na hili tatizo. Mimi ni mjane na sina kazi ya kueleweka, napigania uhai wa mwanangu. Naombeni msaada wenu,” alisema.
“Watanzania wenzangu, naombeni mnisaidie ili niweze kuondokana na hili tatizo. Mimi ni mjane na sina kazi ya kueleweka, napigania uhai wa mwanangu. Naombeni msaada wenu,” alisema.
Akaongeza:
“Wameshachukua nyama za mwanangu na kwenda kupima na baadaye watachukua
zangu ili kuona kama zinaendana, upasuaji ufanyike. Gharama kwa ajili
ya matibabu hayo wamesema ni shilingi 400,000 na mimi sina uwezo.
“Watanzania wenzangu, naombeni mnisaidie ili niweze kuondokana na hili tatizo. Mimi ni mjane na sina kazi ya kueleweka, napigania uhai wa mwanangu. Naombeni msaada wenu,” alisema.
“Watanzania wenzangu, naombeni mnisaidie ili niweze kuondokana na hili tatizo. Mimi ni mjane na sina kazi ya kueleweka, napigania uhai wa mwanangu. Naombeni msaada wenu,” alisema.
SHIRIKI BARAKA
Kumsaidia mhitaji wa kweli huongeza baraka katika kipato, vitabu vitakatifu vinaeleza wazi. Ndugu wasomaji wetu wapenzi, kwa yeyote atakayeguswa na mateso ya familia hii, anaweza kumsaidia chochote mama huyo kupitia simu zake namba 0719 749542 (Tigopesa) na 0762 425973 (M - pesa).
Kumsaidia mhitaji wa kweli huongeza baraka katika kipato, vitabu vitakatifu vinaeleza wazi. Ndugu wasomaji wetu wapenzi, kwa yeyote atakayeguswa na mateso ya familia hii, anaweza kumsaidia chochote mama huyo kupitia simu zake namba 0719 749542 (Tigopesa) na 0762 425973 (M - pesa).
No comments:
Post a Comment