MSANII wa muziki wa kizazi kipya anayeunda kundi la Makomandoo Fredy Wayne ambaye alikuwa akitoka kimapenzi na Jacqueline Wolper anasema ameamua kuachana na msanii huyo na kuamua kuunda uhusiano mpya baada ya Jckline Wolper kuwa anamchanganya na wanaume wengine kimapenzi.
Msanii huyo wa Bongo fleva ameamua kufunguka na kusema kuwa yeye kwa sasa mapenzi yake yote yapo kwa mwanadada Kajala Masanja na anasema haambiwi hasikii juu ya penzi hilo la Kajala. “Siyo siri jamani ndiyo kashaniroga, nampenda na yeye kaonyesha upendo wake kwangu, nipo naye na kuhusu huyo Jack Wolper ni maisha tu, ni rafiki zangu, huwa naona nao katika maeneo tunapiga kiss, ni vitu vya kawaida lakini sasa niko na Kajala,” alisema.
Fredy Wayne |
No comments:
Post a Comment