Hitmaker wa Bomoa Bomoa BABY J ametoa wito kwa vioo vya
jamii hasa wasanii wa kike waliopo katika tasnia ya muziki na filamu
kutojihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya kwani
wanaidhalilisha nchi yetu.
“Well kusema ukweli siwezi kuingilia sana kwa hilo kwa
sababu kila mtu anafanya kitu kupitia yeye mwenyewe na plan zake za
maisha yake, lakini kiukweli kama mwanamke au kama kioo cha jamii sio
kitu vizuri kwa sababu tunachafua majina yetu na pia tunaipeleka vibaya
tasnia zetu hata hivyo tunakandamiza taifa letu la baadae(vijana)”
alisema BABY J kupitia Kipengele cha Chumba Cha Sindano cha Bomba Base
Show kipindi kinachoruka hewani Bomba Fm Radio.
Aidha BABY J amesema jamii inapaswa kuwa makini na maisha
ya sasa kutokana na dunia kubadilika “Kusema kweli kitu kikubwa
nachoweza kukiongea najua watasikiliza Wazee, vijana na watoto nafikiri
kitu kikubwa nachokizungumza ni kwamba binadamu wenzangu wote tuwemakini
kwa sababu sasa hivi dunia kidogo ime-change kuna magonjwa/maradhi
hatari hii na maanisha kwa walio izidi au niliowazidi mimi au tulio
kwenye same age tuwe makini na hii hali”.
Kwa hatua nyingine BABY J amezungumzia ujio wake “Kitu
kingine napenda kuwaambia mashabiki wangu wakae tayari kwa sababu sasa
hivi ni mwaka 2014 kuna vitu vingi vinakuja na watavifurahia kwa hiyo
wavipokee, kuna wimbo natarajia kuuachia japo ni mapema sana kuuongelea,
well studio ambako nitarekodia ni Akhenato chini ya producer Lil Gheto
nafikiri anafahamika”.
No comments:
Post a Comment