Msanii wa muziki nchini, Pancras Ndaki maarufu PNC amesema mpaka
sasa haelewi anaenda wapi na muziki wake baada uongozi unaomsimamia
‘Mtanashati Entertainment’ kutotambua kama upo naye pamoja ama tayari
amepigwa chini.
Wasanii wa Mtanashati Entertainment kushoto ni Happy Balice,Pnc na Dogo Janja
Akizungumza na Bongo5 leo, PNC amesema amekuwa akijitahidi kufanya
nyimbo nzuri lakini anashindwa kufika popote kutokana na uongozi wake
kutokuwa makini na msanii huyo.
“Ulimwengu wa muziki upo simple sana,mimi muziki najua kuimba na
mashabiki wangu wanajua mimi naweza muziki,tatizo kitu kimoja
kinachonifelisha mimi ni uongozi nilionao haueleweki,kama ningepata
uongozi ambao unafuatilia muziki na unaujua muziki ningekuwa mbali
sana.Uongozi wa Ostaz Juma siuelewi elewi kabisa, sijui kuna vitu
vimemkatisha tamaa,hata sielewi muziki wangu unaenda wapi? Yaani
nashindwa kuelewa kabisa,Ostaz yuko busy yaani hata sijielewi kama nipo
na Ostaz ama vipi,” amesema msanii huyo.
“Leo nimeanza kumtafuta nimemtumia meseji, nataka nitambue kama tuko
pamoja ama mimi niendelee na kazi zangu. Mimi nadhani muda wangu umefika
wa kuamka. Watu wamekuwa wakiniuliza kwani bado upo kwa Ostaz? Yaani
wananiona sieleweki,kwahiyo namtafuta nikimpata nikae naye chini niongee
naye nijue kimoja kinachoendelea ni nini. Sishindwi kutunga nyimbo
nzuri za kuwavutia watu. Nyimbo ngapi nzuri zimeshindwa kusimamiwa?
Watu wanajua PNC anaweza fanya muziki mzuri,inauma sana kwanza sikupenda
masuala haya kuyazungumzia kwenye Media ila imenibidi kwasababu watu
wanataka kujua,” amesema PNC kwa uchungu.
No comments:
Post a Comment