Mkurugenzi
wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group,Ruge Mutahaba akitoa
maelezo mafupi kwa Waziri Mkuu Mstaafu,Mh.Frederick Sumaye kuhusiana na
urushaji wa matangazo kwa njia ya kisasa ndani ya studio kuu ya redio
Clouds FM,Sumaye amefanya ziara fupi mjengoni humo na kujionea shughuli
mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo zikiwemo na urushaji wa
matangazo ya redio na Televisheni kwa ujumla.
Mmoja
wa Watangazaji kipindii cha Michezo Clouds FM,kiitwacho Sports Extra,
Ibrahim Masoud a.k.a Maestro akifanya mahojiano mafupi na Waziri Mkuu
Mstaafu,Mh.Frederick Sumaye kuhusiana ushabiki wake mkubwa kwa timu ya
Simba sambamba na migogoro iliyoikumba club hiyo ya Msimbazi
Ruge
Mutahaba akitoa ufafanu mfupi kwa Waziri Mkuu Mstaafu,Mh.Frederick
Sumaye,kuhusiana na Kifaa maalum na cha kisasa cha kurushia matangazo ya
biashara,pichani nyuma ni Mkuu wa Kitengo cha Habari Clouds FM,Joyce
Shebe akisikiliza.
Waziri
Mkuu Mstaafu,Mh.Frederick Sumaye akiwa kwenye chumba cha kurekodia
mahojiano mbalimbali,akiwa amekutana na wadau wa Mfuko wa Dhamana ya
Uwekezaji Tanzania (UTT),pichani kulia ni Afisa Masoko Mwandamizi wa
UTT,Mfaume Kimario na Afisa Masoko na Uhusiano,Bwa.Rahim Mwanga.
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group,Ruge Mutahaba
akitoa maelezo mafupi kwa Waziri Mkuu Mstaafu,Mh.Frederick Sumaye kwenye
moja ya Ofisi za kampuni hiyo,alipofanya ziara fupi mjengoni humo na
kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo zikiwemo na
urushaji wa matangazo ya redio na Televisheni kwa ujumla. pichani kati
anaeshuhudia ni Ofisa Mahusiano wa Clouds Media Group,Simon Simalenga.
Mkuu
wa Kitengo cha Habari Clouds FM,Joyce Shebe akitoa ufafanuzi mfupi kwa
Waziri Mkuu Mstaafu,Mh.Frederick Sumaye alipotembelea kitengo hicho cha
habari na kujionea uandaaji wa habari ya televisheni na redio
unavyofanyika.
Ruge
Mutahaba akimtambulisha Mkurugenzi mwanzake wa Maendeleo ya
Biashara,Sheba Kussaga kwa Waziri Mkuu Mstaafu,Mh.Frederick Sumaye.
No comments:
Post a Comment