MISS Tanzania 2011, Salha Israel ameweka bayana bila ya woga wowote kuwa, kwenye pochi yake hakaukiwi na mipira ya kiume ‘kondom’...
Salha alisema hayo, juzi Jumanne katika mahojiano maalum na Global Publishers.
Katika mahojiano hayo, Salha
aliwekwa mtu kati ambapo alifafanua ishu hiyo pamoja na mambo mengine
ndani na nje ya urembo, bila kusahau tasnia ya sinema ambayo kwa sasa
ameingia kwa miguu miwili.
Swali la msingi lililozaa jibu hilo ni pale alipoulizwa kama aliwahi
kutoa mimba tangu alipoanza kuelea kwenye bahari ya mapenzi, ambapo
alikana kisha akafafanua: “Mimba! Weeeee.... hapana. Sijawahi kupata
wala kutoa mimba.”
Akaongeza: “Mimi natumia kondom bwana, mimba itaingia wapi hapa!”
AMANI: Kama ukienda kwa jamaa na akawa hana kondom unafanyaje?
SALHA:
Na kwa nini asiwe nayo? Lakini siyo tatizo sana, ndiyo maana mimi huwa
nakuwa nazo kwenye pochi muda wote. Nikijua nakwenda kwa jamaa, basi
zinakuwa tayari.
Sitaki
kisingizio, kama atakuwa nazo fine (sawa) but (lakini) akiwa hana natoa
zangu. Unajua mimi ndiye nitakayeingia kwenye matatizo ndiyo maana
nakuwa makini mwenyewe.
AMANI: Kwa hiyo hata sasa hivi hapo unazo kondom kwenye pochi yako?
SALHA:
(Anacheka) Hapana, hapana... kwa sasa sina na hii ni kwa sababu sina
mtu muda huu ila nikiwa naye huwa siachi kuzibeba muda wote.
From:GPL
No comments:
Post a Comment