Blogger Widgets

February 8, 2014

Moja ya Story iliyomake HeadLine Leo ni Hii Kuhusu Huyu Mwanadada ambaye ni msomi wa chuo kikuu Kukutwa akijiuza

Ni aibu iliyoje? Mwanadada ambaye amejitambulisha kuwa ni msomi wa chuo kikuu (jina lipo) ambaye pia ni mwanakwaya chuoni hapo aliyejitaja kwa jina moja la Rei ameaibika baada ya kunaswa usiku mnene akijiuza, Risasi Jumamosi linaifumua.
Mwanakwaya,msomi wa chuo kikuu (katikati), aliyejitaja kwa jina moja la Rei.
Rei alikamatwa katika msako wa polisi katikati ya Jiji la Dar (City Center) hivi karibuni akiwa na kundi la warembo wa vyuo mbalimbali wakifanya biashara haramu ya kuuza miili.
Mrembo huyo ambaye Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishersilimshuhudia, kabla ya kupelekwa kituo kikuu  cha polisi, Wilaya ya Ilala (Central),  alijitetea kuwa yeye ni denti wa chuo kikuu hivyo kitendo cha kupigwa picha alijua kabisa kuwa zitasambaa mitandaoni hivyo itakuwa ni aibu kubwa.
Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers wakichukua picha.
“Kaka naomba usinitoe gazetini au mitandaoni, haya ni maisha tu, itakuwa aibu kwa wanachuo wenzangu,” alijitetea.
Mbali na hayo, mrembo huyo wa haja alikuwa akihaha kuwa kama ishu hiyo itamfikia mchungaji wake, basi hatakuwa na sehemu ya kuficha uso wake.
Pia Rei alijitetea kuwa huwa hajiuzi kila siku na hiyo ilitokea tu kwa bahati mbaya kwani ana biashara zake binafsi.
Alipoulizwa na ‘kachero’ wetu juu ya kanisa au kwaya anayoitumikia alikataa kutaja kwa madai kuwa atalichafua kanisa.
“Wewe ujue tu mimi ni mwanakwaya, hayo mambo ya kwaya na kanisa sitaki kulichafua jina la Mungu,” alisema.
Mwanakwaya,msomi wa chuo kikuu (katikati).
Kwa mujibu wa polisi wa doria waliowanasa warembo hao walidai kuwa Jumatano iliyopita watafikishwa katika Mahakama ya Jiji la Dar (Sokoine Drive) chini ya Hakimu Mkazi, Timothy Lyon kwa kosa la uzururaji kwa kuwa hakuna sheria ya moja kwa moja juu ya ukahaba.

No comments:

Post a Comment