Muigizaji wa filamu, Kajala Masanja amesema afya yake bado
haijakaa vizuri baada ya kunywa kitu chenye sumu kwenye show ya Izzo
Bizness iliyofanyika Club 71, Tegeta Kibaoni Jumapili iliyopita.
Kajala Masanja akiwa katika pozi
“Naendelea hivyo hivyo,” Kajala anayeongea kwa shida ameiambia
Bongo5. “Nilivyoenda kwenye show nimefika nikawa nakunywa ghafla
nikaanza kujisikia vibaya nikawaambia wanipeleke nyumbani. Ghalfa
nikaanza kujitapikia,kujitapikia mpaka nikafika nyumbani nikapelekwa
hospitali nilivyopimwa wakasema nimekula kitu kibaya.”
Kajala amesema hakumbuki kama alikula kitu kingine zaidi ya glasi
moja na Cocktail. Show ya Izzo ilisindikizwa na wasanii kibao wakiwemo
Vee Money, Gosby, Snura Mushi, Shetta, Barnaba Boy, Jux na wengine.
No comments:
Post a Comment