Msanii aliyekuwa chini ya kampuni ya Mtanashati Entertainment,
Pancras Ndaki aka PNC amesema ameamua kuachana na kampuni ya hiyo na
kujiunga na Top Fleva,akidai bosi wake wa zamani amekuwa akimsema vibaya
na kumchafua kwenye jamii.
Akizungumza na Bongo5, PNC amesema haoni sababu ya kuendelea kukaa na
kampuni ambayo haiendelezi muziki wake, bali ni kuchafuana kwa jamii.
“Mimi hajanilipia hoteli zaidi ya kunilipia kodi ya nyumba ya mwaka.
Hayo mambo ya hoteli sijui yametoka wapi?,anasema hivyo ili nionekane
mtu mbaya. Kwahiyo mimi nimeamua kuondoka kwenye usimamizi wake. Kwa
anakuwa mwingi wa ahadi kuliko kutekeleza na kwenye media anatusemea
vibaya. Mimi nimeshajiunga na Top Fleva na tumeanza kurekodi kazi mpya,”
amesema.
Boss wa Mtanashati, Ostaz Juma jana aliiambia tovuti ya Times FM kuwa
PNC na Dogo Janja hawana nidhamu na kwamba pesa alizokuwa anawekeza kwa
wasanii hao ni bora akatoe sadaka.
“Sio yeye tu, na Dogo Janja, wote hawana utovu wa nidhamu kabisa,
mara kumi fedha zangu nizipeleke msikitini au kwa watoto yatima
nibarikiwe kuliko kukaa na watu wasiokuwa na nidhamu,” alisema.
No comments:
Post a Comment