Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ akiwa katika ofisi za GPL akiongea na OFM.
Habari ya Vai kunaswa katika mtego wa kujiuza iliripotiwa na gazeti
damu moja na hili, Ijumaa toleo la wiki iliyopita, ambapo msanii huyo
aliingia mkenge baada ya kukubali kukutana na ‘pedeshee’ mmoja kutoka
mkoani kwa lengo la kumpa uroda kwa malipo ya shilingi 500,000.Akizungumza na Risasi Mchanganyiko juzi, Jumatatu jijini Dar es Salaam, Vai alisema: “Kiukweli lile tukio lilinichanganya sana lakini pia limenipa fundisho kubwa. Nawaomba ndugu zangu na mashabiki wangu wote wanisamehe kwa dhati kabisa.
“Naahidi sitarudia tena ujinga kama ule. Ilikuwa ni tamaa tu. Hivi ninavyozungumza na wewe nipo kwa editor (mhariri) nasimamia editing (uhariri) ya filamu yangu ambayo ipo katika hatua za mwisho kuingia mitaani. Niko bize na kazi, acha niwekeze kwenye ujasiriamali tu. Nawashauri wasanii wenzangu tutulie maana OFM wapo macho.”
Alisema, katika filamu yake hiyo aliyoipa jina la Beautiful Liar amewashirikisha wakongwe Mohammed Fungafunga ‘Jengua’, Hashim Kambi ‘Wingo’ na mastaa wengine kwenye tasnia hiyo na kwamba mashabiki wake wakae mkao wa kula.
No comments:
Post a Comment