Ostaz Juma ameendelea kuongezea petroli kwenye moto aliouwasha
jana. Na sasa amewaamkia wasanii na watangazaji wote wa redio nchini
akisema njaa inawasumbua na ndio maana wamekuwa wakimsujudia..
Hiki ndicho alichokiandika kwenye Facebook:
Naona watu mmeguswa sana mimi kuanika Picha za PNC katika
mitandao et, tatizo wasanii wa tanzania mnanjaa sana kuanzia watangazaji
Radio na wasanii njaa ndio zinazo wasumbua.
Hata mkisema napata pesa kwa utapeli mitandaoni sawa ila ndio pesa
zangu na ndio zinawafanya mnitetemekee na kunitaja kwenye vinyimbo vyenu
visivyokua na ubora. Sawa mimi tapeli naibia watu hilo sikatai nakubali
mimi tapeli ila imekuaje msanii wenu kaja kunipigia magoti?
Wasanii wa bongo njaa sana na mtakufa na njaa zenu. Acheni
muendelee kunyonywa kwa ujinga wenu shule mmezikimbia tatizo. Mnaniona
mimi mbaya kuweka picha Za PNC zimewauma sana eeh. Hahahahahahahahahah
pesa inaongea hata mseme nini.
Naomba nyie mabloger na watangazaj msio kua na taaluma wekeni na hii.
No comments:
Post a Comment