MISS
Tanzania mwaka 2011, Salha Israel amevunja ukimya baada ya kumuweka
wazi mwanaume anayetoka naye, jambo ambalo amejaribu kulifanya siri kwa
muda mrefu.
Miss Tanzania mwaka 2011, Salha Israel.
Salha alifungua kinywa na kubainisha hayo, hivi karibuni alipokuwa kwenye mahojiano na
inayorushwa na mtandao namba moja wa burudani Bongo,
inayorushwa na mtandao namba moja wa burudani Bongo,
Akijibu
swali la mtangazaji aliyekuwa akifanya naye mahojiano, Luqman Maloto,
aliyetaka kujua kuhusu uhusiano wake, Salha alijibu kwa kifupi akisema:
“Yeah! Ninaye mchumba.”
:
“Anaitwa Moses. Ndiye moyo wangu, maisha yangu, kila kitu kwangu.
Nafurahi mwanaume huyu kuja maishani mwangu, maana amekamilisha ndoto
zangu. Najivunia kuwa naye kwa kweli.”
Hata
hivyo, hakutaka kufafanua zaidi kuwa huyo Moses ni nani, anafanya nini
na jina lake la pili, kwa maelezo kuwa ni mapema kufanya hivyo.
Huyu hapa anafafanua zaidi: “Hiyo inatosha, ni Moses. Hakuna haja ya mwanaume yeyote kuwaza tena kuhusu mimi. Nafasi imejaa.”
“Nawashukuru sana Global TV kwa
kunipa nafasi ya kutoa yangu ya moyoni hasa katika kuweka mambo yangu
hadharani, najipanga vizuri kufanya mambo makubwa ya kijamii na siyo
skendo kama watu wanavyochukulia,” alisema Salha ambaye kwa sasa ametia
maguu kwenye tasnia ya filamu za Kibongo
No comments:
Post a Comment