Blogger Widgets

February 26, 2014

Tazama Picha:Wasanii 12 watinga kwenye bunge la katiba



                         

                John Kitime, Simon Mwakifwamba    
Wasanii 12 wakiwemo viongozi toka Shirikisho la muziki, Shirikisho la Filamu, Shirikisho la Sanaa za ufundi, Mtandao wa Wanamuziki Tanzania walifunga safari na kuvamia Dododma na kuwa na mfululizo wa mikutano na wabunge mbalimbali ili kuwashawishi waunge mkono vipengele viwili ambavyo wasanii wanavitaka katika Katiba

                                 Joseph mbilinyi,John Mnyika, John kitime, simon mwakifwamba
wasanii kutambuliwa katika Katiba kama vile walivyotambuliwa Wakulima, wafugaji, wavuvi na wafugaji walivyotajwa

Milliki Bunifu kwa kiingereza Intellectual Property ambamo ndani yake kuna Hakimiliki itajwe rasmi katika Katiba hili litawezesha sheria mwafaka zitungwe katika kuendeleza sanaa na kulinda kazi za sanaa na kazi za ubunifu. Kundi hili limepokelewa vizuri sana na wabunge wote lililokutana nao.
                                                    Simon Mwakifwamba, Yvonne chellyl, kitime
Ni hatua nzuri na historia inajengeka kwa mara ya kwanza katika kupigania tasnia kutambulika kwa maslahi na kutoa ajira kwa jamii kubwa huku ikiwa ni sehemu ya kujenga uchumi usiotegemea madini na vitu vingine, endapo burudani itatambuliwa na kuingia kuwa sekta rasmi tatizo la ajira litapungua kwa asilimia kubwa.

No comments:

Post a Comment