Blogger Widgets

March 8, 2014

Haya Huyu Hapa Roma na Ngoma Yake Mpya ya KKK na Asimulia kuhusu yeye kuingia kwenye siasa

Msanii wa Hip Hop, Roma Mkatoliki amesema kuwa hajawahi kufikiria kama atakuja kuwa mwanasiasa katika maisha yake, ingawa kuna baadhi ya viongozi na wadau mbalimbali wamekuwa wakimtaka agombee Ubunge.
ROMA TUZO
Roma amesema kuwa ameshapokea maoni kutoka kwa viongozi mbalimbali wakimshawishi agombee nafasi ya kisiasa, ila anadai alikataa kwakuwa anatambua nafasi yake ni ipi katika jamii.
“Toka miaka mitano iliyopita nimekuwa nikiendelea kupokea maoni mbalimbali kutoka kwa wasanii wenzangu,wananchi wa kawaida na viongozi wa dini ,viongozi wa serikali, mawaziri wabunge, na kunifuata na kuniambia nigombee ubunge,” ameiambia Bongo5.
“Sijawai kufikiria kuingia katika siasa kugombea ubunge ama kujiHusisha na siasa,napenda nisimame kama msanii kwasababu naamini jukwaa ambalo ninalo ni bora kuliko jukwaa ambalo wanasimama wanasiasa au kuliko mheshimiwa fulani. Mahubiri yangu ninavyohutubia katika muziki inawezekana yana nguvu kubwa kuliko hata mtu fulani, kiongozi ama mbunge wa jimbo fulani. Kwahiyo nafasi ambayo nipo naiona ni nzuri na sijawahi kufikiria kuingia katika siasa.”
ROMA CDM

Hata hivyo Roma amesema kuvaa nguo ya chama fulani haimaanishi kwamba yeye ni mwanasiasa.
“Nyimbo yangu mpya kuna mstari unasema ‘Kambarage hakuwa chadema lakini alivaa ‘track suti’, kwahiyo ni mavazi kama mavazi mengine. Wakati mwingine tunavaa sana jeans, tunaona ngoja leo nivae kanzu, kesho nivae suti, kesho kutwa nivae kitenge, hata shule ya msingi zamani tulikuwa tunanavaa mavazi ya kaki mavazi ambayo hayana tafsiri yoyote. Kwahiyo mimi navaa chochote kile ambacho kitanivutia hata msanii akitoa brand nimeipenda ninaweza nikaivaa bila kuangalia tofauti zetu ama tofauti za watu wengine. Sidhani kama Roma ni mtu ambaye unaweza ukamtafsiri kwa mavazi. Kwahiyo yale ni mavazi ambayo Roma kama Roma alivaa lakini Roma hafungamani na chama chochote cha siasa, mimi nafungamana na sera nzuri, sera ambayo itamkomboa kwa hali kila Mtanzania.”
Jumatatu ijayo, Roma ataachia wimbo wake mpya, KKK.

No comments:

Post a Comment