DIVA wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford, amefunguka kuwa ameamua
kuacha pombe kwa sababu ameona haina faida yoyote kwake zaidi ya
kumzeesha na kumfanya aonekane kama mama mtu mzima.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, juzikati jijini Dar es Salaam,
Shamsa alisema: “Nilikuwa napiga sana mtungi, yaani nilikuwa nikipata
nafasi ya kunywa, napiga balaa lakini naona hakuna cha maana, sanasana
nimeambulia kuharibu umbo langu tu,” alisema Shamsha na kuongeza:
“Nimeamua
kuachana nayo kabisa. Haina faida na mimi. Achilia mbali kupoteza mvuto
wangu lakini pia namaliza fedha nyingi, sitaki, nimesema sitaki tena
pombe.”
No comments:
Post a Comment