Ommy Dimpoz anatarajia kuupeleka muziki wa Tanzania ‘next level’
baada ya wiki hii kushoot video ya wimbo wake mpya jijini London,
Uingereza.
Ommy akiwa na model atakayeonekana kwenye video hiyo
Ommy ameiambia Bongo5 kuwa kwa sasa ni mapema kutaja jina la wimbo huo lakini amedai ni moto wa kuotea mbali.
Ommy akiwa location ya video hiyo
Video hiyo imeongozwa na muongozaji wa video kutoka Nigeria anayeishi
nchini Uingereza, Moe Musa. Muongozaji huyo ameongoza video za wasanii
wengi wakubwa na nyimbo nyingi ni hits. Video hizo ni pamoja Azonto na
Antenna za Fuse ODG, Skelewu ya Davido, Caro ya Starboy ft L.A.X na
Davido, Ukwu ya Timaya na zingine nyingi.
Moe Musa na Ommy Dimpoz
Moe Musa hutoza kuanzia dola elfu 20 kwenye video anazofanya (bila kujumlisha gharama zingine)
Ommy Dimpoz ambaye amekuwa nchini Uingereza tangu Valentine’s Day,
anatarajia kurudi nchini wiki ijayo na atajiandaa na ziara nyingine ya
Muscat na Oman.
From:Bongo5
No comments:
Post a Comment