Blogger Widgets

March 15, 2014

Soma Taarifa ya Watu wanne, Mwanaume mmoja na wanawake watatu kukamatwa na Madawa ya Kulevya kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) Wakielekea Hong Khong

Watanzania wanne (mwanaume mmoja na wanawake watatu) wamekamatwa na kilo 2.2 za heroin kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA). Watanzania hao waliingia nchini Kenya kupitia Namanga na walikuwa njiani kuelekea Hong Kong.

"Tumewakamata Watanzania wanne leo (jana) JKIA. Tumewaweka chini ya uangalizi na tayari wameshatoa vidonge 186 ambavyo tumevifanyia uchunguzi na kudhibitisha kuwa ni heroin," Ngisa aliliambia Shirika la Habari la Uchina kwa simu. Ameongeza kuwa watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani leo Ijumaa.

No comments:

Post a Comment