Muite Chagga Barbie,hivyo ndivyo kila mtu amjuavyo kwa jina lake hilo
maarufu,mrembo huyu kutoka hapa bongo,anayeishi nchini Marekani,ndiye
aliyekuwa anatoka na mkali wa muziki kutoka nchini Kenya,Prezzo na kama
ilivyo kawaida ya
watu maarufu wengi, mahusiano yao hayakuweza
kudumu,mwisho wa siku kubwagana tena kwa kurushiana maneno kupitia
mitandao ya kijamii, ikiwemo twitter,ila baada ya muda ilijulikana kuwa
waliweza kusuluhisha msala wao,ila hiyo haikuwa ishu.
Sasa baada ya mkasa huo wakubwagana na Prezzo,Mrembo huyu alionekana
ku-spend muda mwingi na Davido, msanii maarufu kutoka nchini Nigeria
,wengi wakimjua kama mkali wa skelewu,walionekana pamoja wakati wa
concert ya Davido, iliyofanyika huko mji wa Minneapolis nchini
marekani,na mashabiki wengi kubaki kujiuliza maswali mengi kama ndiyo
tumepata shemeji m’Nigeria hivi sasa hivi au la?.
Davido ametokea kuwa ni moja ya wasanii wakubwa Africa,ameweza
kushinda tuzo mbali mbali zikiwemo,Kora Award, Channel O Music Video
Award, Nigeria Music Video Award, tuzo tatu za The Headies awards, tuzo
nne Nigeria Entertainment Awards, na tuzo mbili za Dynamix All Youth
Award katika muda mchache tu toka aanze ku-make headlines kupitia nyimbo
yake ya skelewu,iliyompa umaarufu mkubwa duniani.
No comments:
Post a Comment