Zile teaser za Weusi zilizokuwa na title ya ‘OTEA’ ambazo
wamekuwa wakiziweka kupitia akaunti zao za mitandao ya kijamii kuanzia
wiki iliyopita, tayari imefahamika kuwa ni ujio wa video ya single yao
mpya ‘Gere.
Nikki wa Pili wa Weusi ameiambia Bongo5 kuwa wameshoot video ya
‘Gere’ Nairobi ,Kenya siku chache zilizopita na director Enos Olik
aliyefanya video ya Jaguar ‘Kioo’.
moja ya screen shots za ‘Gere’
Hapo awali ilikuwa inafahamika kuwa kulikuwa na mpango wa video hiyo
kufanywa na Nisher, lakini Nikki ameelezea sababu za mabadiliko
yaliyojitokeza mpaka kuamua kufanya na Mkenya.
“Bahati mbaya Nisher alikuwa yuko caught up na mambo mengi na
sisi tulikuwa na haraka so tukashindwa, kwasababu Arusha na Nairobi sio
mbali tukavuka tu boda tu fasta.”
Kama wewe unawafollow Nikki Wa Pili, G-Nako au Joh Makini sina shaka umeshakutana na post kama hii:
‘Joh_makini :Otea(gere video) iko tayari kwa yoyote anayetaka xclusive ya siku tano ya video hii..wasiliana na weusi company….’ hii ni post ya Joh Makini Instagram.
Weusi wamesema kabla video ya ‘Gere’ haijatoka wanataka kuifanyia
biashara kwa yeyote anayetaka kuipata exclusive kwa siku tano kabla
haijatoka rasmi iwe ni kampuni, blogs, au mtu binafsi.
“Hiyo ni biashara kwa mfano labda kampuni labda Voda au nani
tunaweza tukawapa wakaweka kwenye page yao labda ya Facebook ikawa
inapatikana pale tu”.
Nikki ameongeza kuwa video ya ‘Gere’ itatoka wiki ijayo.
From:Bongo5
No comments:
Post a Comment