Ikiwa ni miezi miwili imepita toka huduma ya mtume Lesego Daniel wa
nchini Afrika ya kusini ya Rabboni Ministries Centre kuwa maarufu
duniani baada ya waumini wake kula manyasi ikiwa moja ya namna ambavyo
roho mtakatifu alivyowaongoza, bado waumini wa huduma hiyo wanaendelea
kula manyasi na kufanya njia moja wapo ya kupata uponyaji licha ya watu
wengi kupinga ufunuo wa namna hiyo.
Kupitia picha zilizotolewa na huduma hiyo kupitia ukurasa wake wa
facebook, umeonyesha waumini wakikimbilia matawi ya miti na kuanza kula
majani yake, huku mmoja wa waumini aliyefika kanisani hapo kwa mara ya
kwanza amesema amepona jino lililokuwa likimuuma mara baada ya kula
majani, amesema kwamba alifika kanisani hapo kwa mara ya kwanza siku ya
ijumaa akiwa na dawa za kutuliza maumivu pamoja na panado lakini
hazikumsaidia ila majani yalimponya na kwamba akirudi nyumbani mumewe
(ambaye pia mtumishi) atafurahi sana kwa uponyaji huo.
Huduma hiyo ambayo inaongozwa na mtume msomi Lesego Daniel imekuwa
ikipingwa na watu wengi hasa baada ya tukio la waumini kula nyasi huku
pia mtume huyo mda mwingine huwafanyia maombi waumini wake huku akiwa
amewakanyaga migongoni. Licha ya kelele kutoka kwa viongozi wa dini na
makanisa mbalimbali kuwakataza waumini wao na wakristo kuwa makini na
huduma ya mtumishi huyo, ndio kama wamewaruhusu kwenda huko kwakuwa
inasemekana huduma hiyo imeendelea kujikusanyia waumini kila kukicha.
Huduma hiyo ilikuwa ikifanya huduma zake katika majengo ya chuo kikuu
cha teknolojia cha Tshwane kwasasa wamepata enero lao ambalo wameliita
shamba la Rabboni ambalo wanatarajia kuhamia huko jumapili ijayo ya
tarehe 4.
S
|
Waumini wakigombea matawi ya miti ili kupata majani ya kula, huu ni uharibifu wa mazingira nakwambia kha. |
|
Mwenye nguvu anaondoka na majani mengi, kama uonavyo kila mmoja na tawi lake mwe.
|
|
Dada ambaye hapana shaka ndiye aliyeponywa jino. |
|
Dada akitoa ushuhuda huku wenzake wakiuchapa usingizi ambao kila mmoja anajua yupo wapi. |
|
Mtume Lesego Daniel akizungumza huku akiwa amemkanyaga mmoja wa waumini aliyelala chini baada ya maombi. |
No comments:
Post a Comment