Blogger Widgets

December 26, 2012

Ya Wakubwa,Mtoto Jiheshimu:Sababu zinazosababisha mwanamke kuchelewa kutoa ute ute na Jinsi ya kuondoa tatizo anapokutana na Mpenzi wake.



Habari wapenzi wasomaji wangu, ni matumaini yangu kwamba sote tupo salama na tunaendelea kulisukuma kurudumu la maisha salama. Mimi ni msimamizi tu na wala sio Daktari, lakini najua ili suala la ukavu katika uke linawakumba wanawake wengi na hii hupelekea wakati mwingine mzozo katika ndoa zao. Si hivyo tu, ukavu humsababishia mke maumivu na kutofurahia tendo la ndoa au kukataa kabisa, na pia humfanya mume kushindwa kuendelea na raundi nyingize pale inaobidi.

Ukavu huwakuta wanawake wa aina mbili:-
 
  
(1) Wanawake watu wazima waliofikia ukomo wa kupata ujauzito na 
(2) Wanawake ambao bado wana nafasi ya kupata Ujauzito(Mabinti).

Kwa Ujumla ukavu husababishwa na Upungufu wa Ute Ute katika uke unasababishwa na upatikanaji mchache wa homoni za Astojeni. Ukosefu wa homoni hizi hupelekea kutokuwa na unyevu katika uke wakati wa tendo la ndoa, unyevu ukikosekana Tishu za Ukeni huelemewa na kupelekea maumivu kipindi au baada ya tendo la ndoa.   

Tatizo kwa Wanawake Ambao bado hawajafikia ukomo wa Uzazi (Mabinti)
                          Ingawa tatizo hili ni la kawaida kwa wanawake watu wazima wengi, lakini hutokea pia kwa mabinti au wanawake ambao bado hawajafikia ukomo wa uzazi. Kwa mabinti tatizo huweza sababishwa na matatizo ya kiafya, matatizo haya mara nyingi huchochewa na njia za uzazi wa mpango za kisasa mathalani sindano au vitanzi (japo si kwa wote).

                              Pia tatizo kwa wanawake mabinti huweza kusabibishwa na kutokuwa tayari kisaikolojia au hofu katika kichwa chako, mathalani unamwonea aibu mmeo, au kuna kosa umemfanyia na bado una mashaka kuhusu kusamehewa au la, au unajambo linakusuta moyoni (mfano una mpenzi wa nje ambaye ni  mjuzi zidi ya mumeo)


                              Kingine kinachosababisha ukavu kwa mabinti au wanawake ambao bado hawajafikia ukomo wa uzazi ni ukosefu wa Lishe Bora. Hapa ni uwanja mpana kidogo na ndio maana nimeandaa mada ya chakula bora cha kupandisha nyege na kuongeza Ute ute katika Uke Siku zijazo. Ni matarajio yangu kama sababu nilizozielezea kwa uchache zitafanyiwa kazi basi wake zetu watapunguza tatizo hilo. Ingawa kwa baadhi ya watu hushauri hasa wanawake waliovuka umri wa kupata watoto kutumia mafuta ya  
KY GEL
( Siyashauri kwa mabinti)