January 4, 2013

Ile Safari ya Lady Jay Dee kwenda Kilimanjaro Inanukia

Kama unakumbuka mwishoni mwa mwaka jana, mwanamuziki na kiongozi wa Machozi Band, Lady Jaydee alitangaza kupanda Mlima Kilimanjaro mapema mwaka huu wa 2013 ikiwa ni sehemu ya kuwashawishi watanzania na fans wake kuhusu utalii wa ndani, sasa Lady Jaydee ameanza safari hiyo ya kuelekea Mlima Kilimanjaro na siku ya Jumatatu ndo ataanza kuupanda mlima wenyewe.