Mike Sangu akilia kwa uchungu baada ya kuondokewa na dada yake.
Msanii
maarufu wa sinema za Kibongo, Michael Sangu ‘Mike’ amepata pigo la
kuondokewa na dada yake, Salma Said na kujikuta akilia kama mtoto mdogo
na kusababisha watu kuwa na kazi ya ziada kumbembeleza.
Mike
alipatwa na pigo hilo wiki iliyopita baada ya dada yake huyo kuugua kwa
muda mfupi akisumbuliwa na maumivu ya titi moja lililokuwa limevimba
hali iliyosababisha kifo chake katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,
Dar.
Mazishi ya dada huyo yalifanyika Ijumaa iliyopita katika Makaburi ya
Kinondoni, Dar na kuhudhuriwa na watu kibao wakiwemo waigizaji wa filamu
ambapo mkewe, Salome Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ alikuwa na kibarua kizito
cha kumbembeleza Mike anyamaze.
No comments:
Post a Comment