Mwanaume raia wa China ambaye alipata ajali ya kukatwa kabisa
mkono wake wa kulia na mashine ya kiwandani, alilazimika kuunganishwa
mkono huo na kifundo cha cha mguu wake (ankle) kwa muda wa mwezi mzima
ili uendelee kuwa hai wakati akisubiri kufanyiwa upasuaji wa kurudishiwa
mkono huo sehemu yake.
Madaktari waliomhudumia Xiao mara baada ya kupata ajali hiyo Novemba
10, walimwambia hawataweza kuuokoa mkono wake, lakini alipohamishiwa
katika hospitali kubwa masaa saba baada ya ajali ndipo alipoambiwa bado
kuna uwezekano wa mkono huo uliotengana kabisa kuwa hai.
Xiao aliambiwa zoezi la kuurudisha mkono wake sehemu yake linaweza
kufanikiwa, lakini mpaka mkono wake wa kulia utakapopona kabisa. Na ili
kuendelea kuufanya mkono uliokatika uwe hai wakati huo wa kusubiri,
madaktari walisema hawana njia nyingine zaidi ya kuunganisha na ‘ankle’
ya mguu wake.
Desemba 10 ndipo madaktari waliamua kuurudisha mkono wa Xiao sehemu
yake, na wamesema kuwa zoezi la upasuaji huo lilienda vizuri japo kuwa
atahitajika kufanyiwa operations nyingi za ziada ili kuufanya mkono
upone kabisa.
No comments:
Post a Comment