Emmanuel baada ya kupokea kichapo cha nguvu kutoka kwa wanachuo.
Kijana
anayejulikana kwa jina moja la Emmanuel (30), amejikuta akipokea kipigo
‘hevi’ baada ya kukamatwa akiiba katika Chuo cha Theofilo Kisanji ndani
ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa
Kijitonyama, Dar. Tukio
hilo lilitokea hivi karibuni kanisani hapo, mchana kweupe ambapo jamaa
huyo ambaye amekuwa akifika mahali hapo mara kwa mara, alijikuta
arobaini yake ikitimia na hivyo kutiwa mikononi mwa wanachuo ambao kabla
ya kuhoji zaidi, walimshushia kipigo cha mbwa mwizi.
Wanachuo wakikagua baadhi ya vitu alivyokutwa navyo Emmanuel.
“Huyu
ndiye huwa anatuibia humu chuoni na kanisani, kila siku watu
wanalalamika kuibiwa vitu vyao. Juzi tu, kuna watu waliibiwa simu,
wengine fedha lakini hatukujua ni nani aliyekuwa akitufanyia hivyo, sasa
huyu tutamkomesha,” alisema dada mmoja huku akiwa na furaha ya
kukamatwa kwa jamaa huyo.
No comments:
Post a Comment