Masanii wa filamu, Kajala Masanja amedai kuumizwa na watu wanaojiita
‘Team Wema’ kwa kumzushia kuwa anatembea na mume wa zamani wa rafiki
yake, Wema Sepetu na kudai kuwa anatarajia kumtafuta Wema ili kuzungumza
naye.Kajala ameiambia Bongo5 kuwa tangu uzushi huo uanze, bado hajakaa kuzungumza na Wema.
“Mimi ningependa hawa Team Wewa ndio wangezungumza na ndio
wameanzisha. Sina tatizo na Wema, kwahiyo hao ndio wanajua mimi sijui.
Hata bwana wake huyo simjui,mimi aliyeanzisha simjui ila kama unakumbuka
nilianza kuzushiwa ya mume wa Shamim leo wanasema mume wa Wema labda
ndio vinawafurahisha. Yaani mimi sijui chochote,sijaonana na Wema. Wema
alikuwa busy anashoot movie yake na mimi nilikuwa mimesafiri nimeenda
kwa bibi yangu labda sasa hivi aliporudi ndipo nitamcheki tuzungumze,”
amesema Kajala
No comments:
Post a Comment