Steve amesema kuna mtu mmoja anayetumia jina kubuni Tumaini ameendelea kukusanya fedha nyingi kutoka kwa watu mbalimbali na kusema kuwa waache mara moja kwakuwa ni mwizi.
Steve amekielezea kitendo hicho kama wizi usio na aibu kwa familia ya Sajuki iliyopo kwenye majonzi makubwa.Ameongeza kuwa taratibu zote za kukusanya fedha zinaendelea msibani maeneo ya Tabata jijini Dar es Salaam huku yeye na Mike Sango wakihusika na ukusanyaji huo.
MATUKIO YA MSIBANI
Pichani kati ni Naibu Waziri wa Wizara ya
Mawasiliano.Sayansi na Teknolojia,Mh January Makamba
akipata maelezo mafupi kutoka kwa Rais wa Shirikisho
la
Filamu Tanzania (TAFF),Simon Mwakifwamba (wa pili
kushoto) kuhusiana
na mikakati na mipango mbalimbali ya
mazishi ya Marehemu Sadick Juma
Kilowoko a.k.a
Sajuki,nyumbani kwao Tabata Bima,jijini Dar.Aidha kwa
taarifa rasmi kutoka kwa Simon Mwakifwamba ameeleza
kuwa mazishi ya
marehemu yatafanyika kwenye makaburi ya
Kisutu siku ya Ijumaa mapema saa
tano asubuhi.Kuli kwa
Naibu Waziri ni Mkurugenzi wa utafiti wa Clouds
Media
Group,Ruge Mutahaba.na Rais wa Shirikisho la Filamu
Tanzania (TAFF),Simon Mwakifwamba akitoa maelezo
mafupi kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano.Sayansi
na Teknolojia,Mh January Makamba kuhusiana na taratibu
mbalimbali
kuhusiana na msiba huo,huku baadhi ya wasanii
wengine mahiri wa filamu
wakisikiliza kwa makini.
Mazungumzo
mengine ya hapa na pale yakiendelea kufanyika kuhusiana taratibu nzima
za msiba wa Sajuki,ulioko Tabata Bima,jijini Dar.
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF),Simon Mwakifwamba akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano.Sayansi na Teknolojia,Mh January Makamba,kushoto ni Mkurugenzi wa utafiti wa Clouds Media Group,Ruge Mutahaba.
Baadhi ya Wasanii wa wakijadiliana jambo.
Dua ikiendelea kusomwa nyumbani kwa marehemu Sajuki.
Baadhi
ya Watu mbalimbali wakiwemo wasanii wakongwe wa filamu wakiendelea
kuwasili nyumbani kwa marehemu Sajuki mapema leo jioni.
Watu mbalimbali wakiwa wamekusanyika kwenye msiba wa marehemu Sajuki jioni ya leo maeneo ya Tabat Bima,jijini dar.
Mdau
mkubwa wa Filamu hapa nchini Saimon Simalenga akijaribu kutoa maelekezo
mafupi kwa baadhi ya waombolezaji waliofika kwenye msiba wa marehemu
Sajuki mapema leo jioni.
Badhi ya Wadau na Wanahabari wakiwa wamekusanyika kwenye msiba huo.
Ruge Mutahaba akisalimiana na Mkurugenzi wa ASET,Asha Baraka,pichani kati ni Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano.Sayansi na Teknolojia,Mh January Makamba pamoja na Simon Mwakifwamba.
Wakifarijiana.
Vikao vikiendelea
Ruge
Mutahaba akiwa ameongozana Mh January Makamba wakisalimiana na baadhi
ya watu waliokuwa kwenye msiba,walipokuwa wakiwasili
Baadhi ya Wasanii wakibadilishana jambo
Source:Bongo5
Source:Bongo5