Blogger Widgets

January 27, 2013

Yanga Waipiga Prison3-1.Dr.Ulimboka aungana na Mashabiki wa Yanga kuishangilia Timu


 Young Africans leo imeendeleza wimbi lake la ushindi katika mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom baada ya kuichapa tmu ya Tanzania Prisosns kutoka mjini Mbeya jumla ya mabao 3-1, katika mchezo uliofanyika jioni hii katika dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Young Africans ambayo inaongoza ligi kwa kuwa na pointi 32 na mabao 28 ya kufunga, iliingia uwanjani kwa ajili ya kusaka pointi 3 muhimu ambazo imefanikiwa kuzipata.
Kikosi cha mholanzi Ernest Brandts kiliuanza mchezo kwa kasi, na kupata bao la kwanza dakika ya 11 kupitia kwa Jerson Tegete aliyemalizia pasi safi ya kiungo mshambuliaji Saimon Msuva.
Dakika sita baadae dakika ya 17, mshambuliaji wa Elias Maguli aliipatia Prisons bao la kusawazisha kufuatia uzembe wa walinzi wa Yanga kuzembea kumkaba mfungaji aliyekokota mpira toka upande wa pembeni mpaka alipofunga bao hilo.
Didier Kavumbagu alikosa mabao ya wazi dakika ya 7 na dakika 27 huku kiungo Nurdin Bakari akikosa pia bao la wazi dakika ya 38 ya mchezo.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza Young Africans 1-1 Prisons FC.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Yanga kuutawala mchezo hali iliyopelekea kujipatia bao la pili kupitia kwa mlinzi wa kulia Mbuyu Twite aliyemalizia mpira uliokolewa na walinzi wa Prisons  kufuatia piga nikupige ya Nadir Haroub, na Saimon Msuvalangoni mwa lango la Prisons kabla ya mpira huo kumkuta Twite aliyeukwamisha wavuni.
Jerson Tegete aliendelea kuwa mwiba kwa timu ya Prisons baada ya kuipatia Young Africans bao la tatu dakika ya 66, akimalizia pasi safi ya kiungo Nurdin Bakari aliyetanguliziwa mpira na Hamis Kiiza  na Nurdin kuwatoka walinzi wa Prisons kabla ya kumpasia Tegete aliyeukwamisha mpira wavuni bila ya ajizi.
Kama washambuliaji wa Young Africans wangekuwa makini Yanga ingeweza kuibuka na ushindi wa mabao mengi kwani Jerson Tegete alikosa bao la wazi baada ya kuwapinga chenga walinzi wote wa Prisons lakini umaliziaji wake haukuwa mzuri.
Mpaka mwisho wa mchezo Young Africans 3- 1 Prisons FC
Kiungo Frank Domayo aliugua ghafla na kuondolewa katika orodha ya wachezaji ya waliokuwa katika listi ya kuanza na nafasi yake ilichukuliwa na Nurdin Bakari, Domayo alijisikia kizunguzungu hali iliyompelekea daktari wa timu ya Yanga Dr Nassoro Matuzya kufukiria huenda akawa na malaria, baadaye Domayo alijisikia nafuu na kuutazama mchezo wote kwa dakika 90.
Kocha mkuu wa Yanga Ernest Brndts amesema anashukuru timu yake  kupata kwa ushindi katika mchezo wa leo, kipindi cha kwanza wachezaji wangu hawakuwa makini na hawakuzingatia maaelekezo yangu , lakini wakati wa mapumziko niliwaeleza nini wanapaswa kukifanya na hatimaye timu ilibadilika na kuweza kutengeneza nafasi za kufunga mabao mawili japokuwa walikosa nafasi zingine za wazi  
Kambi yetu ya mafunzo nchini Uturuki imetusaidia sana, wachezaji wanacheza kwa kujiamin ila kuna mapungufu madogo madogo yalijitokeza katika mchezo wa leo, benchi la ufundi tumeyaona na tutayafanyia kazi katika michezo itakayofuata alisema "Brandts"

Young Africans: 1.Ally Mustapha 'Barthez', 2.Mbuyu Twite/Juma Abdul, 3.Oscar Joshua, 4.Nadir Haroub'Cannavaro', 5.Kelvin Yondani, 6.Athuman Idd 'Chuji', 7.Saimon Msuva, 8.Nurdin Bakari/David Luhende, 9.Didier Kavumbagu/Hamis Kiiza, 10.Jerson Tegete, 11.Haruna Niyonzima
 
 Dkt. Steven Ulimboka, akijumuika na mashabiki wenzake wa Yanga jukwaani, wakati wa mchezo huo. 
 Mashabiki wa Yanga, wakishangilia bao la Mbuyu Twite.
Beki wa Prisons, Jumanne Elfadhil akijaribu kumzuia winga wa Yanga, Simon Msuva
Msuva akiruka daluga la Elfadhil
Msuva akiwatoka mabeki wa Prisons
Msuva akiwachambua mabeki wa Prisons
Jerry Tegete akimtoka mchezaji wa Prisons, Sino Augustino katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya TZ Prisons Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni hii.
Tegete na Sino
Sino amemgonga kwenye goti Tegete anayeugulia maumivu
Sino anajiandaa kumiliki mpira Tegete akienda chini huku akiugulia maumivu
Tegete akishangilia moja ya mabao yake na Msuva
Tegete na msuva
Wachezaji wa Yanga wakimpongeza Tegete kulia
Hatari kwenye lango la Prisons
Mpira uko nyavuni kulia, kipa wa Yanga Ally Mustafa 'Barthez' akiwa ameduwaa baada ya Prisons kupata bao lao
Kavumbangu akifumua shuti
Kavumbangu akimtoka Elfadhil
Kavumbangu akimiliki mpira mbele ya mabeki wa Prisons
Henry Mwalugala akiwa amelala kuondosha mpira miguuni mwa Nurdin Bakari
Kocha wa Yanga SC, Mholanzi Ernie Brandts 
 
akisalimiana na kocha wa Prisons, Jumanne 
 
 
 
 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga ilishinda
 
 3-1.

Kikosi cha Prisons kilichoanza leo

Kikosi cha Yanga kilichoanza leo

Didier Kavumbangu akimtoka beki wa Prisons Jumanne Elfadhil katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni hii. Yanga ilishinda 3-1.

Kavu amepiga krosi baada ya kupata mwanya