Blogger Widgets

March 1, 2013

Vazi la Nusu Uchi lamuumbua Msanii Aunt Lulu


MSANII wa filamu asiyekaukiwa na skendo, Lulu Semagongo 'Anti Lulu' hivi karibuni alijikuta akiaibika kwenye onyesho la Bendi ya Extra Bongo baada ya kuvamia jukwaa na kuanza kucheza huku akizianika sehemu zake nyeti. 
 
Anti Lulu alikuwa ameongozana na mtangazaji Maimartha Jesse kwenye shoo hiyo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Meeda, Sinza jijini Dar ambapo kila alipokuwa akicheza alikuwa akimwaga lazi kufuatia kigauni chake kifupi alichokuwa amevaa hivyo kuwafanya wanaume wakware wamkosekose kumfanyia kitu mbaya.
 

Katika tukio lingine, Maimartha naye alijikuta akipata aibu baada ya kunusurika kung’oa meno kufuatia viatu virefu alivyokuwa amevaa kumpiga mwereka ambapo kama siyo Lulu kumshika, tungekuwa tunazungumzia mambo mengine.
Licha kunusurika huko, Mai alionekana kutembea kwa shida sana kana kwamba alilazimishwa kuvaa viatu hivyo ambapo kuna wakati wanaume walimzomea hali iliyomfanya akose amani.






Wawili hao walifika ukumbini hapo kulinadi shindano la Kigori wa Manywele ambapo awali lilikuwa likifahamika kwa jina la Kimwana wa Mwanywele.