VIDEO Queen wa Bongo Fleva, Mimah Mohammed ‘Baby Candy’ ameibuka na
kueleza namna ambavyo aliugua malaria kali hadi kudaiwa kuwa amerogwa na
shosti wake, Jacqueline Pentzel.
Chanzo makini kililiambia Amani kuwa hivi karibuni nyota huyo
alichanganyikiwa kwani majini huwa yanampanda kichwani mara kwa mara
huku Jack akidaiwa kuwa ndiyo chanzo cha matatizo hayo.
“Amewehuka kabisa, ukimuona utamuonea huruma na Jack ndiye anayedaiwa kumroga,” kilisema chanzo.
Baada ya habari hiyo kuvuja, paparazi wetu alimtafuta Baby Candy ambaye
alikiri kuumwa pamoja kupata taarifa za uvumi kwamba Jack anahusika
lakini yeye anamshukuru Mungu kwani ameshatibiwa hospitalini.
“Mimi na Jack bado tunaongea vizuri, niliamua kukaa mbali naye kwa
sababu ya maneno mtaani, siwezi kusema alinifanyia kitu kibaya, nilikuwa
nikisumbuliwa na malaria, nimetibiwa hospitali na sasa nimepona,”
alisema.
From:Global publisher
No comments:
Post a Comment