STAA wa
sinema za Kibongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ (pichani) amemtimua mdogo
wake aliyekuwa akiishi naye aitwaye Mary baada ya kunasa ujauzito.
Chanzo
makini kilicho karibu na staa huyo kimepenyeza habari kuwa, Shilole
alifikia maamuzi hayo baada ya kumuonya binti huyo aachane na mwanaume
aliyemjaza mimba hiyo lakini hakusikia hivyo akaona bora amtimue.
“Kamtimua baada ya kumuonya mara nyingi bila mafanikio akaona isiwe tabu bora aepuke aibu,” kilisema chanzo hicho.
Alipoulizwa
kuhusiana na ishu hiyo, mdogo huyo wa Shilole alikiri kutimuliwa na
sasa amehamishia makazi kwa jamaa yake anayefahamika kwa jina la Tonny
Montensi anayeishi Sinza, jijini Dar.
No comments:
Post a Comment