Baada ya Dj Khaled kutokea MTV akitangaza mapenzi yake ya
dhati kuhusu nia ya kumuoa Nicki Minaj, mrembo huyu wa Young Money ameonekana Crustacean Restaurant Los Angeles
Marekani akiwa na pete ya uchumba kwenye mkono wake wa kushoto wakati
alipotoka kula chakula cha jioni na baadhi ya marafiki zake waliosoma pamoja
High school.
Unadhani hiyo pete kavishwa na Khaled????!!! Biiig No…. kwa
mujibu wa Necole hii ni pete ambayo inaaminika alivishwa na boyfriend wake wa
longtime kitambo anaitwa Safaree ambae nae amekua akionekana kavaa pete kama
hiyo ya gold ambayo imesababisha watu waamini pia uwezekano wa ndoa ya siri ya
wawili hawa.
Dj Khaled na huu mpango wake wa kutangaza nia ya kumchumbia
Nicki Minaj aliiambia Power 106 kwamba anampenda sana Nicki Minaj kama ambavyo
wanaume wengi wamekua wakivutiwa kumuoa pia, lakini akasisitiza kama Nicki
atakataa kuchumbiwa na yeye… hakutakua na ubaya, bado ni marafiki…
Namkariri akisema ‘Nicki anaweza kutokua tayari kwa ndoa ila
nitamwambia ninachofeel, hata akisema ndio kwangu au akiniahidi mwakani
nitasubiri tu, sitokata tamaa… nataka watoto’