Toka wimbo mpya wa Vanessa Mdee ‘Come Over’ utoke wiki iliyopita
kumekuwa na fununu kuwa hayuko tena chini ya label iliyokuwa inamsimamia
awali (B Hits Music Group), Vanessa aka Vee Money amethibitisha
kuondoka katika label hiyo na sasa ana management mpya.
Akizungumza katika kipindi cha Showtime New Chapter ya RFA, Vee Money
amesema kwa sasa ana management team ya kwake binafsi ambayo ndiyo
inafanya maamuzi yote kuhusu muziki wake, kazi ambayo hapo awali ilikuwa
ikifanywa na B Hits. Pia amemtaja mtangazaji wa Choice FM, Abby, kuwa
ndiye meneja wake kwa sasa.
“Muziki nafanya sasa hivi nafanya independent zaidi niko under
management ya kwangu peke yangu….na manager wangu ambaye anaitwa Abby
ndio tunafanya all of the decisions kama team.”
Wiki iliyopita Vanessa ametoa single mpya ‘Come Over’ iliyofanywa na
producer Nahreel pamoja na Erasto, ikiwa ndio single yake ya pili baada
ya Closer.
Hata hivyo mpaka sasa Vanessa hajaweka wazi sababu za kuondoka B Hits, label iliyomtambulisha na single yake ya kwanza ‘Closer’.
KWA UPANDE WA MABESTE
Dole singer Mabeste amejiondoa kwenye kundi la B’hitz music group na
kusimama kama solo artist. Haijajulikana wazi kwa nini Mabeste
amejitenga na kundi hilo la B’hitz.
Katika ukurasa wake wa Facebook Mabeste hajaelezea chanzo cha kwanini hayupo tena katika group hilo la BHITS
No comments:
Post a Comment