Blogger Widgets

October 25, 2012

Shekhe Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania wilayani Tunduru avamiwa na Kupigwa Mapanga

Shekh mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania Wilayani Tunduru Alhaji waziri Chilakweche

Na,Steven Augustino,Tunduru

Watu wanaodhaniwa kuwa ni Waislamu wenye msimamo Mkali wa Dini wamemvamia na kumpiga Shekh Mkuu wa Baraza la Waislamau Tanzania Wilayani Tunduru Alhaji waziri Chilakweche na kumsababishia maumivu makali.

Kabla ya tukio Shekh huyo alifatwa nyumbani kwake na vijana na kumuomba watoke nae nje ya eneo la nyumba yake wakidai kuwa wanaomba awasaidie kusuhisha Mgogoro uliokuwa umezuka katika msikiti wa Kitumbini katika Mtaa huo.

Sambamba na tukio hilo pia kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Rajab Abdalah (17) Amelazwa katika Hospitali ya Serikali ya Wilaya ya Tunduru akiwa hajitambui baada ya kushambuliwa kwa mapanga na watu ambao walidaiwa kukimbilia katika tukio la shambulizi la Shekh Chilakwechi.

Mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa manane ambapo katika madai yao vijana hao walimtuhumu Alhaji Chilakwechi kuwa amekuwa akishiriki na kula vyakula vya wakirsto. 
 

Akiongea kwa taabu alihaji chilakwechi alidai hakuwa na ubaya nao na wala hajwahi kugombana na mtu hali ambayo inamshangaza na anaiomba Serikali ifuate mkondo wake kwa wahusika.

kuhusu tuhuma za yeye kushiriki katika shughuli za dini katika madhehebu ya wakristo alidai kuwa hicho siyo kitu cha ajabu kwa viongozi wa dini na kuongeza kuwa wao kama viongozi wa dini huwa na ushirikiano na huitana na kutembeleana kwa vile dini hailuhusu uhasama miongoni mwao.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma Bw. Deusdedth Nsimekli amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa jeshji la polisi linaendelea na uchunguzi ili kujua kiini cha tukio hilo.

Aidha kamanda Nsimeki alikiri pia kufahamu matukio ya udini yanayo endelea Wilayani Tunduru nakuongeza kuwa jeshi limejipanga kuhakikisha kuwa wanadhibiti vitendo hivyo.

1 comment: