Akiwa
anaojiwa na East Africa Radio kipindi cha SUPER MIX na mtangazaji
Zembwera msanii mkongwe Lady Jay Dee alikuwa na wakati mgumu sana
alipokuwa akiulizwa unamuelezeaje msanii Mangwear, Jide alikuwa mwenye
huzuni sana na alikuwa akijibu huku akitokwa na machozi. Kuhusu show
yake iliyokuwa inatakiwa ifanyike kesho kutwa Ijumaa Lady Jide alisema
imebidi aisogeze mbele kidogo mpaka msiba huu upite kwanza ndipo atasema
tarehe rasmi.