Mwanamziki anayefanya vizuri kwenye
gemu ya Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ siku za nyuma alitoa kauli
ya kuwa mchumba wake ambaye ni mtangazaji wa Runinga ya DTV, Peniel
Mungilwa ‘Penny’ ana ujauzito wake na kwamba amemnunulia ‘mkoko’ (gari)
la mamilioni ya shilingi kwa ajili ya kwenda nalo kliniki kama utakuwa
mfutaliaji mzuri wa story zetu basi utakuwa umeshaisoma hii sasa Penny
ameifungukia kauli hiy
Baada ya penny kulizwa juu ya ujazito wa Mwanamziki Diamond alioneka kushangzwa sana na kauli hiyo na kupaniki ghafla
Alisema amekuwa akisoma habari za
‘mimba’ yake kupitia magazeti lakini hajawah kuulizwa na mwandishi
yeyote, jambo linalomshangaza sana.
Na hivi ndivyo ilivyo kuwa katika maongezi na mwandish kutoka GPL
Penny alisema: Namshangaa! Ni mimba ipi kwanza?uhusiano wangu na Diamond unaninyima raha kutokana na maneno ya watu.
Penny: Mh! Yaani sijui hata niseme
nini, nashangazwa sana na hizi habari, nazisikia tu halafu mimi mwenyewe
mhusika sijapewa nafasi ya kuzungumza.
Unajua sijazoea maisha haya ya kila wakati kuzungumza na waandishi. Naomba mniache, nani aliwaambia kuwa mimi nina mimba?
Penny: Kama ni Diamond muulizeni yeye mwenyewe! Mbona nakosa raha jamani?
Funguka: Vipi mna mpango wa kuoana na Diamond?
Penny: (kwa hasira) Hizo ni ishu
zangu binafsi, kama tutaoana au hatuoani ni mipango yetu, sioni sababu
ya kutangaza kwenye media.
Funguka: Unaichukuliaje kauli ya mama
mkwe wako, yaani mama Diamond? Inadaiwa alisema hatambui uhusiano
wowote wa mtoto wake na mwanamke mwingine hadi atakapofunga ndoa.
Penny: Tafadhali sana, sitaki kuzungumzia habari kuhusu mama Diamond. Kwa hilo ‘no comment.’
Funguka: Vipi lakini, unainjoi kuwa na uhusiano na Diamond?
Penny: (Akakata simu).
Funguka: Haloo… haloo!
Hata hivyo mapaparazi wetu walipojaribu kumpigia simu tena hakupokea licha ya kuita kwa muda mrefu mpaka kukatika yenyewe
From:GPL