SAKATA LA DIAMOND NA UWOYA ,UWOYA AMWAGA CHOZI
KUFUATIA
habari iliyoripotiwa na gazeti tumbo moja na hili, Amani wiki iliyopita,
ikiwa na kichwa cha ‘DIAMOND AFICHUA KISA CHA KULALA NA UWOYA!’,
mwigizaji Irene Uwoya amemfungukia mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond
Platnumz’ kwa kitendo chake cha kuanika uhusiano wao.
Kwa
mujibu wa mtu wa karibu wa Uwoya, baada ya habari hiyo kuingia mtaani na
kuzua gumzo kubwa, mwanadada huyo alishindwa kupiga misele mjini na
kujikuta akiwaza hadi akamwaga chozi akijuta kuwa karibu na Diamond.
Baadaye Uwoya aliamua kuzama kwenye ukurasa wake katika mtandao wa kijamii wa Instagram na kuandika:NA GPL
“Kuna saa najiuliza kwa nini ukimwamini mtu ndiyo anakugeuka...kwa nini ukiwa muwazi watu wanakuchukulia vibaya?
“Leo
nimeumia sana kuliko siku zote...sijaamini mtu niliyemwamini kumuona
kama rafiki yangu anaweza kuongea sh*t kuhusu mimi...au najiuliza
siruhusiwi kuwa na rafiki wa kiume?
“Lakini saa nyingine nakaa chini nasema God ...u know me better.”
Uwoya
alipoandika maneno hayo ikawa kama amechochea kuni kwenye moto ambapo
mashabiki wake walimshambulia kwa maneno makali kuwa aliporipotiwa mara
ya kwanza na gazeti hili alikanusha sasa mbona mwenzake kaanika ukweli?
Uwoya na
Diamond walidaiwa kuwa ‘wanatoka’ kwa muda mrefu na walifanya jitihada
za hali ya juu kuuficha ukweli kuhusu uhusiano wao lakini ilipofika
Machi 25, mwaka huu, gazeti hili liliwanasa chumbani katika hoteli moja
iliyopo Mbezi Beach ufukweni mwa Bahari ya Hindi, Dar.
No comments:
Post a Comment