Blogger Widgets

February 19, 2014

Soma Alichojibu Msanii Linah Baada yeye kuwa na Ujauzito wa Muhindi Mmoja town


MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya, Estelinah Sanga maarufu kama Linah, anadaiwa kupewa ujauzito na kijana mmoja wa Kihindi anayejulikana kwa jina moja la Nagar.

Chanzo cha uhakika kimeliambia gazeti hili kuwa msichana huyo aliyeibukia kutoka kituo cha kukuza vipaji cha THT, amekuwa karibu na Mhindi huyo anayedaiwa kuishi Mbezi jijini Dar es Salaam kwa muda mrefu sasa na kwamba mimba hiyo imeonekana kumfurahisha sana msanii huyo.
“Huyu Nagar ni mpenzi wake wa muda mrefu na inaonekana hii mimba ameipenda sana. Kila siku anamsifu huyo mpenzi wake,” kilisema chanzo hicho kilichodai kuwa wawili hao wamekuwa wakiambatana pamoja katika sehemu mbalimbali za starehe.

Chanzo hicho kilisema Linah alikutana na mdosi huyo katika harakati zake za kimuziki na kwamba jamaa ameoza mno kwa binti huyo, mkali wa albamu ya Atatamani.
Linah alipopigiwa simu mara ya kwanza hakupokea, lakini baada ya kutumiwa ujumbe mfupi wa maneno na kuulizwa kuhusu suala hilo, alipiga simu na kukanusha vikali tuhuma hizo.
“Nani kakwambia kama nina mimba? Hakuna kitu kama hicho, hayo ni maneno ya watu wanasambaza mtaani, mimi hata sijui wananitaka nini,” alisema.
Alipoulizwa kama hata yeye amewahi kusikia habari hizo, alisema anazisikia na kusisitiza kuwa siyo za kweli. Lakini alipotakiwa kusema kama anamfahamu Nagar, alimtaka mwandishi kuachana na habari hizo.
“Wewe si umeuliza habari za mimba? Sasa hayo mengine yanatoka wapi, ulichotaka kujua nimekujibu, hayo mambo mengine achana nayo,” alisema bila kufafanua zaidi

No comments:

Post a Comment