Blogger Widgets

May 22, 2014

Leo Kupitia Mitandao Mitandao Mbalimbali Hasa ya Facebook na Twitter nimeona wakipost Sana Baadhi ya Mistari ya Nyimbo Mpya Ya Stamina Mzee wa Punchline.Sasa Pata Nafasi za Kusoma Mashari Yote ya Nyimbo Hiyo ft. Walter Chilambo Pamoja na Kudowload Nyimbo Nzima

10152385_836184846411037_2006060161427459043_n
Song: mguu pande mguu sawa
Artist: stamina ft walter chilambo
Studio: one love fx
Producer; tiddy hotter
Song writer: stamina (verse),walter (choruss)
Intro;stamina
Yeaaah,,,u know what tiddy
One love fx again men
Iz moro town in da house
Shorwebwenzi on this one
Vers 1(stamina)
Peleka kitanda batani,kama unapenda ukeshe bar/
Sista duu muda hausimami,hata uivulie nguo saa/
Ishi kiushujaa,kama umepanga kambi ya jeshi/
Kati ya maarufu na star,maarufu anaongoza kwa deshi/
Ewe raisi wa wanyama,fanya sensa usisahau/
Mfuasi aliyesaliti chama,huku mjini bonge la nyau/
Tunza bible sio irizi,ufalme wa mbingu hauna fensi/
Ndo maana akifaga mzinzi,mazishi hatufanyi gesti/
Chagua kilicho best,kati ya copy na kupaste/
Je Yule aliyefeli maisha na class alifeli test?/
Hakuna demu anayejiuza,hicho ndo nikijuacho/
Nachojua wanakodisha,unatumia huondoki nacho/
Bitozi msaka mchumba,usiforce unapotemwa/
Piga goti kwa muumba,ikibidi akuumbe tena/
Mguu mmoja pande,mwingine urudishe sawa/
Hiyo ndo ishara ya kiafande,ya kuweka mambo sawa/
Chorus(walter chilambo)
Naamini kama nyuma ulikosea rudi
Weka mambo sawa na plan b
Unaweza fanya bora zaidi (muda bado)
Mguu pande(mojaaaaa)mguu sawa(mojaaaaa)
Nyuma geuka(moja mbili tatu mojaaa)…..x2
Mguu pandeeee(mojaaaaaa)mguu sawa(mojaaaa)
Nyuma geukaaaaaa.
Verse 2(stamina)

Mjini wanyama kibao,cha ajabu wanakula unga/
Mawazo ya vichwa vyao,dingi afe warithi nyumba/
Ewe kengeza,chunga usimcheke chongo/
Cha msingi muombe ebeneza,akupe vision yenye michongo/
Saka chaka kila sehemu,maana pesa ina machale/
Nyie mnaowinda mademu,hivi mna nyota ya mshale?/
Mnyamazie mshenzi,ukimjibu tu anatuna/
Hadi shoga nae ana mpenzi?,kweli madem mna huruma/
Mziki umejaa stress,ambazo haziishagi kwa pombe/
Mastar wamewekeza desi,wanakufa hawana hata ng’ombe/
Underground chondechonde,usiache shule kisa mziki/
Usuperstar una mabonde,na miteremko ya dhiki/
Yesu anarudi lini?,hilo swali ndo ujiulize/
Sio stamina utaoa lini,nitajibu tu niko bize/
Mguu mmoja pande,mwingine urudishe sawa/
Hiyo ndo ishara ya kiafande,ya kuweka mambo sawa/
Chorus(walter chilambo)
Naamini kama nyuma ulikosea rudi
Weka mambo sawa na plan b
Unaweza fanya bora zaidi (muda bado)
 Mguu pande(mojaaaaa)mguu sawa(mojaaaaa)
Nyuma geuka(moja mbili tatu mojaaa)…..x2
 Mguu pandeeee(mojaaaaaa)mguu sawa(mojaaaa)
Nyuma geukaaaaaa.
Vers 3(stamina)
Usitupe mayai kiholela,zalisha ili uache chata/
Maisha baiskeli ya delela,ukiinama chako unapata/
Kumpa kibogoyo mnofu,kisa nyama bei aghali/
Ni sawa na kumteta kipofu,huku kifikra anaona mbali/
Hakuna zali la mentali,kwenye sayari ya kupendwa/
Mlevi mnywa safari,je unajua unapokwenda?/
Acha mashauzi,sista duu genge linalipa/
Ujanja sio kwenda south,au china ili ukawe striper/
Mapenzi ni kutendwa,mpendaji jiamini/
Sharo ukiona unapendwa,ujue una nyota ya ukimwi/
Ni sawa na uote,usiku una kiss na jini/
Halafu uamke ujikute,una lips stick kwenye ulimi/
Unahitaji akili,sio mashavu yenye dimpoz/
Mwanaume jasiri,hajichubui kisa ana pimpoz/
Mguu mmoja pande,mwingine urudishe sawa/
Hiyo ndo ishara ya kiafande,ya kuweka mambo sawa/
Chorus(walter chilambo)
Naamini kama nyuma ulikosea rudi
Weka mambo sawa na plan b
Unaweza fanya bora zaidi (muda bado)
 Mguu pande(mojaaaaa)mguu sawa(mojaaaaa)
Nyuma geuka(moja mbili tatu mojaaa)…..x2
Mguu pandeeee(mojaaaaaa)mguu sawa(mojaaaa)
Nyuma geukaaaaaa.

No comments:

Post a Comment