Baada ya kuachana na Diamond Platnumz, Peniel Mwingila aka Vj
Penny ameendelea mbele na maisha yake, lakini amekanusha kuwa na mpenzi
mpya kama ambavyo wengi wamekuwa wakidhani hasa wanapomuona yuko karibu
na mwanaume mwingine.
Leo Penny ameamua kuvunja ukimya wake na kukanusha habari
zilizoenezwa katika mitandao ya kijamii kuwa ana mpenzi mpya aitwaye
Rummy, hiki ndicho alichokiandika:
“Ah come on people!!?? Kweli mi ni mkimya ila sasa mnavuka mipaka,
seriously?? Am so disappointed to see posts that Rummy is my new
boyfriend..mnatoa wapi hizi rumours? Just because sijibu shutuma
natupiwaga haimanishi mimi sio binadamu kila siku mnanizushia mapya its
not funny maisha yangu kutwa mnayafanya uwanja wa kutunga kitu, yes
mnatukana na hakuna tusi jipya nawaacha ili mjifurahishe but now u r
crossing the line, I have alot of respect for Rummy he is my homeboy na
marafiki pia wa kiume nisiwe nao? Wengi wanajua rummy ni nani yangu ila
making these stories aint cool at all. Enough has a limit! Nitukaneni
all u want ila msinisingizie vitu sijafanya its just not fair at all.
Kama new boyfriend ntaweka mwenyewe mapenzi hayajifichi ila tusizushiane
uongo, nayavumilia mengi ila hili too much.”
No comments:
Post a Comment