Kendrick
Akiongea na Bongo5, Mabeste amesema tayari amemfungulia mwanae akaunti kwenye mitandao ya kijamii ambako huko ndiko atakuwa akipromote maduka hayo.
“Mwezi ujao tu anaweza akaanza sababu nimemtengenezea page yake na blog yake ndio inakuja ambayo itakuwa inatangaza biashara kupitia social networks. Yale maduka yatakuwa yanamlipa mwisho wa mwezi,” alisema.
Mabeste
Katika hatua nyingine, Mabeste amesema amemfungulia mwanae email ambayo huweka picha zake kila siku akimpiga.
“Toka day one mama yake akiwa na ujauzito, nilikuwa nampiga picha hadi amejifungua, akikua ntampatia password na story ya maisha yake yote anakuja kuikuta kule.”
No comments:
Post a Comment