MSANII wa kike wa filamu Bongo anayetamba na filamu za Asili
Swahiliwood Husna Chobis ‘Avana’ amedai kuwa hataki kuzaa na mwanaume wa
Bongo kwa sababu wengi ni walaghai, na kwa sababu yeye ni maarufu
anapata wakati mgumu kumjua ni mwanaume gani anaweza kuwa mkweli kwake,
anaweza kuwa anamtamani kwa sababu ya jina lake tu.
.
.
“Sitaki
kuzaa na mwanaume asiyeeleweka wengi ni walaghai anakutumia tu kisha
anakutelekeza sasa wana nini? Bora kwa nchi za wenzetu kuna kuwa na ndoa
za mikataba unajua kabisa nitakuwa na mtu huyu kwa muda fulani nizae
naye au tule raha tu mwazo mwisho,”anasema.
Avana ambaye anatamba na filamu ya Gawa iliyotengenezwa na Mussa
Banzi anasema kuwa tayari alishawahi kuumwa na nyoka baada ya kuolewa na
kusumbuliwa hadi kuachana na mumewe jambo ambalo hataki litokee katika
maisha yake tena na hataki kuzaa na mwanaume wa Bongo labda kwa ndoa ya
mkataba kama Ulaya.
No comments:
Post a Comment