UZINDUZI
wa albamu ya Mtenda Akitendewa ya bendi ya Extra Bongo usiku wa jana
umefana kwenye ukumbi wa Dar Live, maarufu kama Uwanja wa Taifa wa
Burudani, Mbagala, Dar es Salaam.
Kivutio
zaidi kilikuwa kiongozi wa bendi ya Extra, ‘Kamarade’ Ally Choky
aliyeingia ukumbini na gari la kukimbizia wagonjwa mahututi hospitali,
maarufu kama Ambulance ukumbini.
Ambulance
hiyo ilisindikizwa na pikipiki zaidi ya 30 zile ambazo mjini tunaziita
bodaboda, ambazo zilipofika mbele ya jukwaa zilifanya fujo za kutosha
hadi mojawapo kudondoka na kumjerujhi dereva wake.
Choky aliibuka kwenye mlango wa Ambulance akiwa peke yake na kupanda jukwaani moja kwa moja kuanza kuimba.
Kwa
kiasi fulani ilikumbushia enzi zile za msisimko wa muziki wa dansi
nchini kwa kiwango cha juu gwiji huyo alipokuwa akiingia ukumbini na
Farasi, TingaTinga na kadhakika na kusababisha mpinzani wake mkuu enzi
hizo, Banza Stone ampige kijembe “Kwenye Starehe Kijiko kimeingiaje”.
Lakini
jana Banza hakuwa mpinzani wa Choky, bali alikuwa mmoja wa wanamuziki
waliyeimba naye jukwaa moja pamoja na Prince Mwinjuma Muumini ‘Kocha wa
Dunia’ na bendi ya Tanzania One Theatre (TOT) upande wa Taarab.
Choky
alipagawisha mashabiki kwa nyimbo kadhaa zilizosindikizwa na sebene la
nguvu lililokuwa linapikwa na wataalamu wa ala wakiongozwa na Ephraim
Joshua katika gita la besi.
Utamu
zaidi katika shoo zilizovurumishwa na wanenguaji mahiri na wasiozeeka
viuno wakiongozwa na Super Nyamwela na Maria Sharapova.
Kabla
ya Choky kupanda jukwaani, bendi ya TOT Taarab ikiongozwa na Malkia
Khadija Omar Kopa na Abdul Misambano ‘Super Rocky’ ilikata utepe na
baadaye wakapanda Mashujaa kabla ya wanamuziki wa Bongo Fleva Fleva Amin
na Linah kutoka THT kuvamia jukwaa.
Idadi
ya watu waliohudhuria onyesho hilo haikuwa kubwa
sana, lakini si haba kwa hadhi ya sasa ya Choky na wote waliomsindikiza viliendana na ukumbi ulipendeza kiasi chake.
FROM:bin Zuber
Wapinzani wa zamani; Ally Choky kushoto akiimba na Banza Stone jana Dar LIve |
Ally Choky akishuka kwenye Ambulance |
Ambulance ya Choky ilivyopokelewa ukumbini |
Ajali; Boda boda hii ilikula mwereka na kujeruhi dereva wake |
Choky na mnenguaji wake |
Choky na Muumin Mwinjuma |
Maboda boda yakiongoza msafara wa Choky |
Wanenguaji wakifanya yao jukwaani |
Bin Zubeiry anapendwa na wengi sehemu nyingi,hapa nikiwa na mshakj wa Global Publisher kitengo Mawasiliano, ambaye ni kati ya wanaoendesha tovuti ya Global |
Viongozi wa makundi ya TMK Wanaume Halisi, King Kiboya kulia na TMK Wanaume Family Said Fela kushoto walikuwepo |
Mashujaa Bendi wakifanya yao jukwaani |
Khadija Kopa TOT kushoto akipagawisha mashabiki |
Amini na Linah kushoto wakifanya yao jukwaani |
sana, lakini si haba kwa hadhi ya sasa ya Choky na wote waliomsindikiza viliendana na ukumbi ulipendeza kiasi chake.
No comments:
Post a Comment