Blogger Widgets

February 13, 2013

Siri Kubwa ya Mzee majuto ya Kuonana na Mh.Jakaya Kikwete

 
Stori: Mwaija Salum
STADI wa sanaa za maonesho nchini, Amri Athuman ‘King Majuto’ amesema ameamua kumtafuta Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete kwa sababu ana siri nzito anayotaka kumpa.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko juzi jijini Dar es Saalam, mkongwe huyo alisema ni kweli anahitaji msaada wa trekta  ambao anaweza kupewa na wasaidizi wake, lakini ana mengi anayotaka kumwambia rais.
 
Amri Athuman ‘King Majuto’
“Nina mashamba makubwa yenye hekari 11 huko Muheza (Tanga), natarajia kulima mazao ya biashara lakini sina uwezo wa kununua trekta ndiyo maana nataka rais anisaidie. Lengo langu ni kuonesha mfano kwa wasanii wengine. Sanaa ina mwisho wake, siwezi kuigiza milele ndiyo maana nahitaji sasa kuwekeza kwenye kilimo.
“Pamoja na hilo nina mengi ya siri ninayotaka kuzungumza na rais kuhusu sanaa yetu. Nitamtafuta kwa juhudi zote na nina imani nitafanikiwa kuonana naye maana najua rais wetu ni mtu wa watu,” alisema King Majuto.
King Majuto ni msanii wa vichekesho aliyejizolea umaarufu mkubwa Bongo, amewahi kutwaa tuzo mbalimbali ikiwemo ya Mkali wa Kuchekesha iliyotolewa na gazeti hili mwaka juzi.