Tukio hilo lilitokea Jumanne iliyopita saa 12 alfajiri ambapo ilidaiwa kuwa Jack alikuwa chumbani na mwanaume huyo ambaye ni mpangaji, wenzake wakipeana maraha.
Picha tofauti juu zikionesha mke wa mtu na mgoni wake katika fumanizi liliotokea.
Imedaiwa
kuwa, wawili hao walikuwa wakimtegea Ngosha akitoka kwenda katika
shughuli zake, Jazira alikuwa akizama katika chumba cha rafiki yake na
kufanya mchezo wa kikubwa.
KERO YAVUJISHWA NA MAJIRANI
Wapangaji wenziye na Jack wamedai kuwa, mke huyo wa mtu ambaye ana miezi miwili tangu aolewe kutoka mkoani Tabora, amekuwa kero katika nyumba hiyo kwani amekuwa akipiga kelele za kimahaba nyakati za asubuhi ambapo watu wengi wanakuwa wakielekea kazini.
Wapangaji wenziye na Jack wamedai kuwa, mke huyo wa mtu ambaye ana miezi miwili tangu aolewe kutoka mkoani Tabora, amekuwa kero katika nyumba hiyo kwani amekuwa akipiga kelele za kimahaba nyakati za asubuhi ambapo watu wengi wanakuwa wakielekea kazini.
Hii ni nyumba waliyopanga wafumaniwa hao.
“Hata
sisi wanawake tunaoishi nyumba hiyo tuna waume zetu tunawalilia lakini
kinachotusikitisha mwenzetu anamlilia Jazira badala ya mumewe ambaye
anakuwa amekwenda kazini,” alisema mmoja wa wapangaji wa nyumba hiyo.MLINZI ABUMBURUA
Imeelezwa kuwa, siku hiyo mlinzi wa msikiti alikwenda kumwamsha Ngosha kwenda kusogeza gari lake ili watu wapite na alipofika katika chumba chake, alikuta mlango wa sebuleni ukiwa wazi lakini hakukuwa na mtu, ila chumbani kwake kulisikika redio ikizungumza kwa sauti kubwa.






















