Blogger Widgets
Showing posts with label Simulizi. Show all posts
Showing posts with label Simulizi. Show all posts

December 12, 2013

Wengi Leo wamesikitishwa na Ni Habari ya Huyu Jamaa aliyepufuliwa macho yake Baada ya kusadikiwa kutembea na mke wa Polisi


Elias John, mkazi wa Kigamboni jijini Dar, (28) baada ya kupofuka macho.
AMA kweli haki hakuna.


Katika hali ya kusikitisha sana, kijana mmoja Elias John, mkazi wa Kigamboni jijini Dar, (28) amejikuta katika wakati mgumu wa kupofuka baada ya kuchomwa sindano inayodaiwa kuwa na sumu kufuatia kujihusisha kimapenzi na mwanamke anayedaiwa kuwa ni mke wa askari Polisi.Akizungumza hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Elias alidai alikumbwa na mkasa huo mwaka 2011 wakati akiwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke aliyemtaja kwa jina moja la Amina, ambaye pia alijihusisha na polisi aliyemtaja kwa jina moja la James, aliyekuwa akifanya kazi katika kituo cha Polisi cha Kilwa Road, jijini Dar es Salaam.

“Polisi huyo alikuwa akinifuata mara kwa mara na kuniambia kuwa niachane na mwanamke huyo, lakini kwangu ilikuwa ngumu kwa sababu tulipendana sana,” alisema kijana huyo.

Alisema siku ya tukio, akiwa kijiweni, polisi huyo akiambatana na wenzake, walifika na kumkamata bila kosa lolote na kumpeleka katika kituo kidogo cha polisi Mianzini, Temeke.

 

May 27, 2013

Endelea na Simulizi ya HATOOLEWA KAMWE sehemu ya Tatu Chini ya Utunzi wa ABDULMALIK SIRAJ,,,,,Ona Matokeo Yanafuata Baada ya Bi. Eliza kajifungua Mtoto wa Kike Ikiwa ni Muda Mrefu Kila Mimba Yake Inaharibika




SEHEMU YA TATU Mtunzi: ABDULMALIK SIRAJ
 Simulizi:NA HATOOLEWA KAMWE


****************
Ndipo nesi wazam akamtishia mzee kyashama kama iwapo hatoacha kupayuka kwa fujo atamtoa nje kwani alikua anawapigia kelele wagonjwa jambo ambalo lilimfanya mzee kiashama awe mpole atulie kama maji mtungin au ungezania ananyolewa kwajinsi alivyo nyea huku akikitazama kichanga chake...ndipo nesi alipo mgeukia mwanamke eliza na kumuuliza kisa ni nini!....eliza alisita kuongea akainua macho na kumuangalia mme wake machoni kwa muda mchache kisha akakigeukia kichanga chake na kuanza kukisemesha kama vile anamshtaki mume wake...''mwanangu hivi babaako ni wa kunikaripia na kunikaripia mbele za watu eti tu analazimisha uitwe KOKUSIIMA jina la mamaake mzaz kisa alimuahidi mtoto wa kwanza wa kike atakua mwajina wake...ss mwanangu uoni kama hayo majina ni yakizamani sana mimi nataka uitwe SUZANNA ..eti ndo kosa langu ilo mwanangu ndo niadhirike kias hiki kweli..''...maneno yale yalizua simanzi ndani ya moyo wa mzee kyashama akidi kunyong'onyea na kuinamisha kichwa chake kama mchicha ulonyauka kwa kupigwa na jua...ndipo nesi alipoingilia kati na kusema kuwa sio vibaya kwa mtoto kuwa na mjina mawili kwa ushaur tu jina la kwenye cheti chake cha kuzaliwa atumie SUZANNA... Kauli ile ya nes iliondoa ubishi na kulejesha fulaha kati ya wawili hao.....

****************

SUZANNA ni mtoto pekee wa mzee kyashama aloonyeshwa mapenzi ya dhati kutoka kwa wazazi wake walokua wakimtunza na kumlinda kama mboni ya jicho...jambo hilo lilimfanya suzi aish kwa furaha na kujivunia kuzaliwa ndani ndani ya nyumba ya mzee kyashama!..alipofikisha umri wa miaka tisa alianzishwa elimu ya msingi katika shule ya msingi TUMAINI..punde tu baada ya kuanza shule mschana suzi alikutana na kijana aitwae ERICK... Erick hakuwa mbali sana na alipokuwa akiishi suzi..erick alivutiwa sana na uzuri wa msichana suzi jambo lilimfanya ajiweke karibu sana na suzi,nakujikuta akiwa tayari kujitoa kwa namna yoyote ili mradi tu amfurahishe suzi..wawili hao walijikuta wakiwa karibu sana jambo liliwafanya hata wazazi kutoka pande zote mbili kufahamiana na kujenga urafiki pia...erick alimpenda sana suzi ila hakuwahi kumwambia..kwa upande wa suzi ilikuwa tofauti alimchukulia erick kama rafiki tu..suzi hakumpenda erick kutokana tofauti za kimuonekano,erick alikua anasura mbaya af alikuwa mweusi sana..wanafunzi wenzia walikua wakimtania kwa kumuita

May 26, 2013

Endelea na Simulizi ya HATOOLEWA KAMWE sehemu ya Pili Chini ya Utunzi wa ABDULMALIK SIRAJ



SEHEMU YA PILI
Mtunzi: ABDULMALIK SIRAJ
 Simulizi:NA HATOOLEWA KAMWE
********************

Mzee Kiashama alijikuta anakuwa mlevi wa kupindukia kutokana na kukosa mtoto kwasababu ya matatizo ya mimba kuharibikia tumboni aliyokuwa nayo mke wake Eliza.Siku moja mwanamke Eliza alikua akifagia uwanja unaozunguka nyumba yao ambapo pembeni kidogo ya mlango alikuwepo Mzee Kyashama akirekebisha sturi kwakuigongelea misumali zaidi ili iimalike.Ndipo Mke Wake Eliza alianza kujihisi kama anataka kutapika naghafla akaanza kukimbia kama kibelenge kuelekea kando kidogo ya nyumba na kuanza kutapika huku ameinamisha mgongo wake pamoja na kichwa Huku mkono ukibaki kifuani!.jambo hilo lilimshtua mzee kyashama naye akainuka harakaharaka na kutupa nyundo chini na kuanza kutembea kwa hatua ndefundefu na za harakaharaka huku akitweta kuelekea pale mke wake alipojiinamia..akamfikia na kuanza kumuuliza unatatizo gani mke wangu huku akihemea juujuu akiwa amemshika mgongoni..mke wake hakumjibu bhali alizidi kutoa mafundo ya matapishi kutoka mdomoni mwake uku akizidi kulegea kwa kukosa nguvu!..hali hiyo ilizidi kumtia kiwewe mzee kwa hofu kwamba huwenda akaja kumkosa mke wake kipenzi..palepale akajawa na wazo la kukimbia kuelekea ndani na kurudi akiwa amebeba jagi lenye maji kiasi na kuanza kumuhudumia mke wake kipenzi..ambapo mwanamke Eliza alikunywa yale maji na mengine akayatumia kusukutua mdomoni kisha kuyatema!..mzee kyashama alimkokota mkewe taratibu mpaka alipomfikisha chumbani na kumlaza kitandani huku akimpepea kwa kutumia mfuniko wa Plastiki..taratibu mpaka mke Wake  Eliza akachukuliwa na usingizi..baada ya kama nusu saa Eliza alishtuka kutoka usingizin na kugundua kuwa mme wake amekaa pembeni ya kitanda chake huku akimuangalia kwa huruma...ndipo mzee kyashama akamshika kwenye paji la uso nakumuuliza kiutaratibu kwa sauti ya chini ''vipi mke wangu unaendelaje?''. Eliza naye akajibu kiutaratibu ''naendelea vizuri mume wangu ila kuna kitu nataka nikufahamishe!''..ukimya mfupi ukatawala,mzee kyashama akabadisha mkao na kumgeukia akiwa amemuangalia usoni kwa makini kisha akamwambia ''ondoa hofu mke wangu ongea chochote mkewangu kwamoyo mkunjufu nitakipokea!!

May 23, 2013

Hii Hapa Sasa Ile Simulizi ya Kusisimua "NA HATOOLEWA KAMWE" Sehemu ya KWANZA



 Simuliz:NA HATOOLEWA KAMWE
 Mtunzi: ABDULMALIK SIRAJ
Sehemu Ya: KWANZA
****************


Ilikuwa siku ya juma nne asubuh mida ya saa tano mnamo tarehe 7/5/2013 nikafunga safar kuelekea kwa jiran yangu maeneo ya tandale kwa tumbo aitwae BIBI KUNUKA nipokaribia mlangon
i kwake niliskia harufu kali sana ikitekenya pua zangu ila ikabidi nipige moyo konde na kujongea karibu kabisa na mlango na nikaanza kubisha hodi...hodii hodii (gongongong)...nilibisha zaidi ya dakika kumi hama bibi hajazoea wageni mara nikaona mlango ukifunguliwa chuiiii ...hapo ndo harufu ya uvundo na maharagwe yalichacha ikatia fola hata bila kuuliza nikawa nishafahamu sababu za yeye kuitwa Bibi kunuka...mlango ulipofunguliwa nikaona sura bibikizee ikitoa macho kwamshangao!..ndipo nikakohoa kidogo kisha nikamsalimia ''Shikamoo bibi''..bibi akiwa ananiangalia kwa makini kama vile ananifananisha akaniitikia ''Marhaba mjukuu wangu''...akanambia wewe sio mgeni machoni mwangu wewe si mtoto wa mwenyekiti!?...nikacheka kidogo..nikamwambia bibi mimi sio mtoto wa mwenyekiti mimi jiran yako kila mara nakukuta hapa nje umekaa nakusalia...bibi akasema uzee nao huu...kimya kifupi kikatawala  nikawa bado nimesimama nje ndipo bibi akasema...mjukuu wangu ngoja nikuletee mkeka ukiingia ndan kwangu utaugua mafua kuna harufu kali!..ngoja nikuletee mkeka tukae wote hapa nje!...bibi akaingia ndani punde tu akarudi na mkeka ulochakaa sana kwa matobo na viraka kibao!...tulipo kaa chini nikamkabidhi mfuko wa nailon ambamo ndani yake palikuwemo chapati mbili na soda ya kopo...bibi alipofungua mfuko na kuona vilivyomo nikamuona anachukua chapati harakaharaka nakaishambulia mara akaanza kukuhoa chapat imemniga anatapatapa kama anataka kukata roho...kuona hali hile mimi nikaogopa nikaifungua soda nikamnywesha...akainywa kwa fujo na yenyewe ikampalia ngoja aanze kutapika sasa!..bibi katapika vitu havieleweki vina rangi ya kijani nikaogopa huku kichwani nikijiuliza huyu bibi alikua anakula majan ya mbuz au...baadae nikahisi labda ndo nyongo kama watu wanavyosema kutapika nyongo...ikabidi niingie ndan kumtafutia maji ya kunywa...lalalala nilikuta harufu iyo ndani hakueleweki kumbe ule mkeka ndo huwa analalia hana kitanda wala godoro nikachota maji kwenye mtungi nikampelekea...akanywa maji akatulia kwa muda...kisha akaniuliza ulikua unashida gani kijana?


***********************


Nikamjibu!...Bibi mimi ni mwandishi wa simulizi kama tamthilia pamoja na riwaya!!..akaniuliza kwahiyo ulitaka nikusaidie nini?..akaniuliza!..nikamwambia kabla ya yote bibi naomba nikuulize!..kwaunyonge akanijibu...uliza tu mjukuu wangu!...nikamuuliza..''bibi mbona unaishi pekea yako tena kwa tabu sana kwani watoto na wajukuu wako wapi?''..nilimuona bibi kajiinamia kama anatafakari akanigeukia kuniangalia..ndipo nilipo gundua kuwa macho yamebadilika na kuwa mekundu utadhan amevuta bangi au msubah...nikaogopa ukunikijiuliza..huyu bibi ni mchawi kweli au watu wanamsingizia..mara akajiinamia na kuangua kilio..mpaka wapita njia walikua wakiniuliza!..umemfanyaje bibi yako?..sikuwajibu nilibaki kimya mpaka bibi alipo maliza kulia na kutulia kisha akaniambia mjukuu nashindwa nianzie wapi ...kiufupi mimi ndo mjukuu mimi ndo mtoto navilevile mimi bibi....alipomaliza kuyaongea hayo kwa unyonge akawa kimya kwa muuda kisha nikamuuliza...''bibi jina lako kamili unaitwa nani!?..akanitazama uson kisha akanijibu..''jina langu kamili naitwa SUZANA PATRICK..nimtoto wa kwanza wa marehem Mzee Patrick ila baba yangu huyo alijulikana zaidi kama Mzee Kyashama...!