Elias John, mkazi wa Kigamboni jijini Dar, (28) baada ya kupofuka macho.
AMA kweli haki hakuna.
Katika
hali ya kusikitisha sana, kijana mmoja Elias John, mkazi wa Kigamboni
jijini Dar, (28) amejikuta katika wakati mgumu wa kupofuka baada ya
kuchomwa sindano inayodaiwa kuwa na sumu kufuatia kujihusisha kimapenzi
na mwanamke anayedaiwa kuwa ni mke wa askari Polisi.Akizungumza
hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Elias alidai alikumbwa na mkasa huo
mwaka 2011 wakati akiwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke aliyemtaja
kwa jina moja la Amina, ambaye pia alijihusisha na polisi aliyemtaja
kwa jina moja la James, aliyekuwa akifanya kazi katika kituo cha Polisi
cha Kilwa Road, jijini Dar es Salaam.
“Polisi huyo alikuwa akinifuata mara kwa mara na kuniambia kuwa niachane na mwanamke huyo, lakini kwangu ilikuwa ngumu kwa sababu tulipendana sana,” alisema kijana huyo.
Alisema siku ya tukio, akiwa kijiweni, polisi huyo akiambatana na wenzake, walifika na kumkamata bila kosa lolote na kumpeleka katika kituo kidogo cha polisi Mianzini, Temeke.

“Polisi huyo alikuwa akinifuata mara kwa mara na kuniambia kuwa niachane na mwanamke huyo, lakini kwangu ilikuwa ngumu kwa sababu tulipendana sana,” alisema kijana huyo.
Alisema siku ya tukio, akiwa kijiweni, polisi huyo akiambatana na wenzake, walifika na kumkamata bila kosa lolote na kumpeleka katika kituo kidogo cha polisi Mianzini, Temeke.