.

>>
Autaja
wimbo wa Joto Hasira akiwa na Prof Jay
>>
Asema
litakalokuwa na liwe na hatarudi nyuma
Siku
chache baada ya kutoa wimbo mpya wa Joto Hasira, staa wa muziki, Judith Wambura
‘Lady Jaydee’ ameonyesha kuwa na hasira za ukweli baada ya kushutumu kituo cha
redio kuwa kinatoa upendeleo kwa baadi ya wasanii na ‘kuwabania, wengine.
Kupitia
ukurasa wake katika mtandao wa Twitter wa
twitter.com/JideJaydee, msanii huyo hajataja jina la kituo hicho lakini
inavyoonekana hatua hiyo imefikiwa baada ya wadau hao ‘kuupotezea wimbo wake
huo mpya aliomshirikisha Joseph Haule ‘Prifesa Jay’
Jaydee
ameonekana kuwa na hasira na kuandika baadhi ya maneno kama ifuatavyo:-
·
Redio ya watu isipopiga nyimbo za
wasanii wa watu ila za wasanii wao tu, wasiopendwa na watu. Ni kweli nimelamba
sumu, lakini hainidhulu Nakunywa maziwa daily, I will survive.
·
Kili me if u can, am on Fire, siogopi
Ng’ooooo Jipangeni.
·
2013 no more bullshits, we fight mpk
jasho la mwisho.
·
Mmetiwa petrol inanuka mioyo
imeshawawaka kabla ya kutiwa kibiriti. Maamuzi magumu yalishafanywa na wenye
roho za kutu fanyeni ku top up.
·
Tuki stuck ndo mwisho wetu na adui
anashangilia, ni kupambana tu mpk mwisho radio ziko nyingi mbona.
·
@Profesa_Jay Iwe Joto au Baridi lazima
kushinda mbwai, mbwai tu. Hakuna kuremba.
·
Anaedai kuianzisha bongoflava aliapa
kuiua bongo flava Sasa hata wasioijua Hip-hop nao wana beef na Bongo flava!
Damn!!
·
My name is Judith Wambura Habash!! Hio
imeandikwa kwenye passport. Gmorning.
·
Vinyoka nyamazeni acheni Anaconda
aongee.
·
Hee! Kuna wajinga wanadhani nili tweet
nikwa nimelewa, nilimaanisha na msimamo ni huo. Stasema ooh kuna mtu ka hack ac
yangu nooo it’s me.
·
Kuna DJ flani alikuwa akipiga nyimbo
nilizoshirikishwa akifika sehemu nilioimba mimi anakata verse yangu nimtaje??
